Home » » NAIBU WAZIRI NISHATI SUBIRA MGALU ASEMA VIJIJI 54 MKOANI PWANI KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME WA REA AWAMU YA TATU

NAIBU WAZIRI NISHATI SUBIRA MGALU ASEMA VIJIJI 54 MKOANI PWANI KUNUFAIKA NA MRADI WA UMEME WA REA AWAMU YA TATU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Naibu Waziri wa Wizara mpya ya nishati Subira Mgalu akizungumza na watendaji wa shirika la umeme Tanesco Mkoa wa Pwani pamoja na wakandarasi baada ya kukagua mradi wa REA awamu ya tatu uliopo maeneo ya sofu mlandizi Wilayani Kibaha mkoani Pwani alipofanya ziara yake ya kikazi ya siku moja kwa ajili ya kujionea mwenendo mzima wa ujenzi.(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Naibu Waziri wa nishati Subira Mgalu wa kati kati akipata maelezo kutoka kwa Meneja wa Tanesco Mkoa wa Pwani Martin Madulu wa kushoto katika alipotembelea kituo cha usambazaji wa umeme kilichopo Mlandizi.
Naibu Waziri wa Wizara mpya ya nishati Subira Mgalu akipata ufafanuzi kutoka kwa wakandarasi wa mradi wa umeme wa REA awamu ya tatu katika eneo la Msufini Mlandizi Wilayani Kibaha Mkoa wa Pwani.
Naibu waziri mpya wa Nishati Subira Mgalu akisikiliza kwa umakini maelezo kutoka kwa Meneja wa tanesco Mkoa wa Pwani Martin Madulu wa kushoto mara baada ya kutembelea kituo cha umsambazaji wa umeme kilichopo Mlandizi ikiwa ni ziara yake ya kikazi yenye lengo la kukagua miradi ya nsihati ya umeme 

NA VICTOR MASANGU, PWANI

VIJIJI vipatavyo 54 katika mkoa wa Pwani ambavyo wananchi wake walikuwa katika hali ya sintofahamu kutokana na kukaa gizani kwa kipindi cha muda mrefu hatimaye wanatarajia kupata na kunufaika na nishati ya umeme wa uhakika ifikapo mwezi machi mwaka 2018 baada ya kukamilika kwa mradi wa kusambaza umeme vijiji (REA) awamu ya tatu.

Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa wizara ya nishati Subira Mgalu baada ya kufanya ziara yake ya kikazi ya siku moja katika Wilaya ya Bagamoyo pamoja na Wilaya ya Kibaha mkoani Pwani kwa ajili ya kutembelea baadhi ya miradi ya REA ambayo inatekelezwa kwa awamu ya tatu pamoja na kujionea changamoto mbali mbali zinazowakabili.

Pia Magalu amesema kuwa lengo la serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais Dk. John Pombe Magufuli ni kuhakikisha inapeleka huduma ya uhakika kwa wananchi wake pamona na maeneo mengine yenye kutoa huduma za kijamii na kubainisha kuwa wanatarajia ifikapo mwaka 2021 vijiji vtote nchini view vimefikiwa na huduma ya nishati ya umeme.

Aidha Naibu Waziri huyo alipotembelea kituo cha uzalishaji wa umeme kilichopo maeneo ya Mlandizi aliliagiza Shirika la ugavi wa umeme Tanesco kuhakikisha wanajipanga vizuri ili kuweza kupunguza malalamiko ambayoyamekuwa yakitolewa na baadhi ya wananchi kuunguza vitu vyao majumbani kutokana na tatizo la kukatika katika umeme kila mara bila ya kutoa taarifa.

“Jamani viongozi wangu wa Tanesco kumekuwepo na baadhi ya malalamiko ambayo yamekuwa yakitolewa na wateja kuhusina na hii hali ya kukatika katika kwa umeme mara kwa mara bila ya taarifa hali amabyo inasababisha wakati mwingine wananachi hao kuunguza vitu vyao hivyo katika hili mimi nawaomba mbadilike na mlifanyie kazi katika kuhakikisha lawama hizi zinaondoka kabisa na nina imani mtalifanyia kazi,”alisema Mgalu.

Kwa upande wake Meneja wa Shirika la ugavi wa umeme (Tanseco ) Mkoa wa Pwani Martin Madulu amesema kuwa kukamilika kwa mradi huo wa REA awamu ya tatu utakuwa ni mkombozi mkubwa katika suala zima la nishati ya umeme kwani wanatarajia kuwafikiza zaidi ya wateja 5000, na kuongeza kuwa mradi huo umegharimu kiasi cha shiingi bilioni 5.

Meneja Madulu aliongeza kuwa lengo la Tanesco ni kuhakikisha kwamba wanaboresha zaidi huduma ya nishati ya umeme hususan katika maeneo ya vijijini kwa lengo la kuweza kuwafikia wananchi wengie ambao wataweza kupata fursa ya kutumia nishati hiyo katika kuendeshea shughuli zao mbali mbali za kimaendeleo.

Mhandisi mkuu ambaye anayesimamia miradi ya umeme wa vijijini (REA) katika Mkoa wa Pwani Leo Mwakatobe amesema licha ya kujitahidi katika kunga miundombinu mipya kwa ajili ya nishati hiyo wanakabiliwa na chanagmoto kubwa ya kuwepo kwa baadhi ya wananchi kugoma kuhama kwa ajili ya kupata njia ya kupitsiha mradi huo hivyo kuwapa wakati mgumu katika utekelazaji wa majukumu yao.

“Katika miradi hii ya kusambaza umeme vijijini kwa kweli baadhi ya maeneo bado tunakabiliwa na changamoto kubwa ya wananchi kuwa wagumu kupisha eneo kwa ajii ya kuweza kupata njia ya kupitisha nishati ya umeme, hivyo inatupa wakat mgumu sana katika kufanya kazi zetu na wengi wao wanadai fidia ya kulipwa lakini katika maradi huu hauna fidia kitu kikubwa ni kutupa ushirikiano katika kufanikisha zoezi hili,”alisema Mhandisi Mwakatobe.

KUKAMILIKA kwa mradi wa umeme vijijini awamu ya tatu (REA) katika Mkoa wa Pwani utaweza kuvinufaisha vijiji vipatavyo 154 ambavyo baadhi ya vingine vilishapatiwa umeme huo katika awamu ya kwanza pamoja na ya pili.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa