PWANI KUJENGA VIWANDA VITATU VYA MADAWA NA BAADHI YA VIFAA TIBA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Na Mwamvua Mwinyi, Kibaha

SERIKALI mkoani Pwani, imeitikia wito wa serikali ya awamu ya tano ya kujenga viwanda vya madawa na baadhi ya vifaa tiba ambapo inatarajia kuwa na viwanda hivyo vitatu hali itakayoondoa adha ya kuagiza madawa nje ya nchi .

Aidha imekemea tabia inayofanywa na baadhi ya wawekezaji ya kutoa ajira kwa watu kutoka nje ya nchi na kuwabania fursa hiyo wanaPwani ama watanzania.

Akielezea masuala ya uwekezaji na ajira ,wakati wa ziara yake ya kutembelea viwanda mjini Kibaha ,mkuu wa Mkoa wa Pwani,mhandisi Evarist Ndikilo alisema Viwanda vya madawa vitawezesha kuokoa mamilioni ya fedha yaliyokuwa yakitumika kununulia madawa nchi jirani na nje.

Alieleza viwanda vitatu vinajengwa Mkoani Pwani ikiwemo Kairuki Pharmaceuticals industry Ltd ,Zinga pharmaceuticals ambacho kitajengwa kwa ubia na waislael na kipo mbioni kuanza kujengwa na Bahari pharmaceuticals .

"Tunaikitia wito wa rais Dk.John Magufuli ,lakini pia tangu kipindi cha nyuma tumejipanga kujenga viwanda hivyo ,kupitia ziara hii tunawathibitishia wananchi tunaunga  mkono kauli ya serikali yetu"alifafanua Ndikilo.

Pamoja na hayo ,mkuu huyo wa mkoa alieleza ,zipo fursa mbalimbali  za uwekezaji  lakini vijana na wazawa wanashindwa kukimbilia fursa hizo.

Ndikilo alisema wazazi na vijana bado hawajatambua kujipanga kukuza elimu na ujuzi wao kwa ajili ya kujipatia ajira kirahisi.

Alitoa rai kwa wawekezaji ,kuacha kuwanyima ajira wazawa na watanzania ambao wanaujuzi na sifa za kufanya kazi .

" Haiwezekani tunajenga viwanda vingi lakini vijana ,waTanzania na wanaPwani hawanufaiki na ajira zinazopatikana,haikubaliki"alisisitiza Ndikilo.

"Sidhani kama Pwani ama Tanzania nzima haina wenye sifa na ujuzi,hivyo aliwataka wawekezaji hao watoe kipaombele kwa watanzania wenye uwezo .

Ndikilo alisema amepokea taarifa uwekezaji wa standard gauge eneo la Soga hawatoi ajira hata ya udereva jambo ambalo analichunguza na atakapopata uhakika watachukua hatua zinazostahili.

Aliwataka kununua vifaa vya ujenzi kama nondo ndani ya nchi ,kwani taarifa waliyompatia kwenye ujenzi wa Kairuki Pharmaceuticals industry Ltd kuwa wananunua nondo huko Uturuki .

Alisema kipo kiwanda cha Kiluwa ambacho kinatengeneza nondo zenye ubora hivyo wanunue katika viwanda vya ndani ya nchi.

Nae mkurugenzi  mtaalamu wa Kairuki Pharmaceuticals eng.Valency Assenga alisema ujenzi wa mradi huo ulianza machi 10 mwaka huu na mkandarasi ni Petra Construction Ltd Ltd na unatarajiwa kumalizika Novemba 2018.

Alielezea kazi zote zinaendelea kwani zipo hatua ya awali ya ujenzi na mpaka kukamilika ujenzi wa awamu ya kwanza kiwanda hicho kitagharimu bilioni 3.9 " #

Eng .Assenga alitaja changamoto kuwa ni miundombinu ya barabara,mradi kusuasua kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha na ucheleweshwaji wa uunganishwaji wa umeme.

Mkurugenzi wa halmashauri ya Mji huo ,Jennifer Omolo akizungumzia suala la mipango miji alisema wameanza zoezi la kupima mji muda mrefu  na wanaendelea na zoezi hilo .

Omolo aliwataka watu waache kujenga na kufanya biashara kiholela bila kupangwa ,na kuwashauri waone watalaamu wa mipango miji ofisi ya mkurugenzi ili  kupewa maelekezo ya kupata vibali .

MWENYEKITI UVCCM MKOA PWANI AWATAKA VIJANA KUKITUMIKIA CHAMA KIPATE USHINDI WA KISHINDO MWAKA 2019/2020

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro (katikati) akizungumza na viongozi na wajumbe chama hicho wa Wilaya ya Mafia mkoani Pwani leo,Kiongozi huyo yupo katika ziara ya kutembelea jumuiya za umoja wa vijana wa Mkoa huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Mafia,Amina Tuki wengine kulia ni Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Mlao na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Mafia,Hassan Pango. Picha zote na Elisa Shunda
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman na Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani, Ramadhan Mlao (kulia) wakielekea kupanda ndege kuanza safari kuelekea wilayani Mafia.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman na Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Mlao (kulia) wakiwa ndani ya ndege safarini kuelekea wilayani Mafia kwa ziara ya kutembelea umoja wa vijana.
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman na Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani, Ramadhan Mlao wakiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mafia tayari kuanza kwa ziara yao.

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro akilakiwa na mwenyeji wake Mwenyekiti wa UVCCM wa Wilaya ya Mafia,Amina Tuki (kulia) mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Mafia tayari kuanza kwa ziara yake.

Wenyeji wakiwaongoza wageni kutoka nje ya uwanja wa ndege wa Mafia.
Katibu Tawala wa Wilaya ya Mafia,Gilbert Sandagula akitoa ufafanuzi wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya na Halmashauri kwa ujumla jinsi inavyosaidia vijana wa wilaya hiyo kunufaika na mikopo na miradi mbalimbali inayotolewa na ofisi hizo kwa vijana. Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro akiulizia mambo mbalimbali yahusuyo vijana wa Wilaya ya Mafia kwa uongozi wa wilaya hiyo ofisini hapo. Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Mafia,Hassan Pango,akizungumza wakati Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro na Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Mlao walipowasili katika ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Mafia kupokea taarifa ya usaidizi wa ofisi hiyo katika kuwasaidia vijana wa wilaya hiyo kwenye mikopo ya asilimia 4%.
Katibu wa Mbunge wa Mafia na Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya Mkoa wa Pwani,Fakh Seif akizungumza na akielezea masuala mbalimbali yanayofanywa na mbunge wa jimbo hilo katika kuwasaidia vijana wa wilaya ya Mafia.


Wajumbe wa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Mafia wakifuatilia kwa makini mkutano huo.
 
Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mafia (UVCCM),Amina Tuki akizungumza katika mkutano huo na Wajumbe wa Baraza la Umoja wa Vijana wa chama hicho.


Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro (katikati) akizungumza na viongozi na wajumbe chama hicho wa Wilaya ya Mafia mkoani Pwani leo,Kiongozi huyo yupo katika ziara ya kutembelea jumuiya za umoja wa vijana wa Mkoa huo. Kushoto ni Mwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Mafia,Amina Tuki wengine kulia ni Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Mlao na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Mafia,Hassan Pango.
Wajumbe wa Baraza la Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Mafia wakifuatilia kwa makini mkutano huo. Katibu wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mafia (UVCCM), Ally Omary Hassan akikabidhi risala ya umoja huo kwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro (Kulia) katika mkutano na wajumbe wa baraza UVCCM la wilaya ya Mafia. Anayeshuhudia Katikati ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mafia (UVCCM),Amina Tuki
Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Mlao akiwasisitiza wajumbe wa baraza la UVCCM Wilaya ya Mafia kwa kushirikiana na viongozi wao katika kuhakikisha wanaimarisha chama hicho ili kishinde kwa kishindo uchaguzi ujao wa serikali za mitaa ambao ndiyo sahihi ya ushindi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. Kushoto ni Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mafia (UVCCM),Amina Tuki. Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro akimkabidhi Mwenyekiti wa UVCCM wa Wilaya ya Mafia,Amina Tuki (kushoto) vitabu vya kanuni 100 na kadi za umoja wa vijana 200 kama zawadi kwa ajili ya jumuiya hiyo ya vijana ya Wilaya ya Mafia. Wanaoshuhudia kulia ni Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Mlao na Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Mafia,Hassan Pango. Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro (aliyejifunika kitambaa rangi ya njano) na Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,,Ramadhan Mlao (kushoto kwake) wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Mafia. Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Mlao akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mafia,Mohamed Faki (kushoto) baada ya kumalizika kwa shughuli za mkutano na wajumbe wa baraza la vijana la UVCCM la Wilaya ya Mafia. 
 Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Mlao akiwa kwenye picha ya pamoja na Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wazazi ya Chama Cha Mapinduzi wa Wilaya ya Mafia,Mohamed Faki (kushoto) baada ya kumalizika kwa shughuli za mkutano na wajumbe wa baraza la vijana la UVCCM la Wilaya ya Mafia.


 
 Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro (aliyejifunika kitambaa rangi ya njano) na Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,,Ramadhan Mlao (kushoto kwake) wakiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wa Wilaya ya Mafia.





Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi Mkoa wa Pwani (UVCCM),Charangwa Seleman Makwiro.




Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa Pwani,Ramadhan Mlao akibarizi na kujionea uzuri wa fukwe za bahari katika Kisiwa cha Mafia.




NA ELISA SHUNDA,MAFIA .

VIONGOZI wanaounda Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilayani Mafia wametakiwa kujitoa kwa nguvu,mali na rasilimali zao katika kukitumikia chama hicho na kuhakikisha kinafanya vizuri katika uchaguzi ujao wa serikali za mitaa mwakani na uchaguzi mkuu 2020 ili CCM katika wilaya hiyo kiibuke na ushindi wa kishindo.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Pwani, Charangwa Selemani Makwiro wakati alipofanya ziara wilayani humo leo ambapo katika kuhakikisha vijana wa wilaya hiyo wananufaika na serikali ya Dk.John Pombe Magufuli amepata fursa ya kutembelea ofisi ya wilaya na halmashauri ambapo amekutana na uongozi na kupewa maelezo ya mnufaiko wa vijana wa Mafia katika asilimia 4% ya mikopo na miradi inayotolewa na uongozi huo kwa vijana hao.

Mwenyekiti Makwiro amewaeleza vijana hao kuwa wao ndiyo nguvu ya chama na kuwataka kusimama ngangari kama viongozi na vijana wa CCM kwa kutumia nguvu,mali,akili na rasilimali zao zote katika kuhakikisha chama hicho kinapata ushindi wa kishindo katika uchaguzi ujao wa mwakani wa serikali za mitaa ambapo ndiyo msingi wa ushindi wa uchaguzi mkuu wa madiwani,ubunge na urais hivyo ni jukumu lao vijana kukipigania chama katika maandalizi ya uchaguzi huo.

“nimefarijika siku ya leo kukutana na viongozi na vijana wa CCM wa Wilaya hii ya Mafia napenda kuwausia na kuwakumbusha vijana wenzangu mmeomba nafasi za uongozi kwenye maeneo yenu hivyo basi unapoomba nafasi katika chama hiki usitarajie labda kuna hela utapata au uwe kibaraka wa kiongozi Fulani ili maisha yako yaendelee hapana umeomba nafasi ya uongozi kwa ajili ya kuwatumikia vijana wenzako ni jukumu lako kama kiongozi sasa kutumia nguvu zako,akili,mali na rasilimali katika kukitumikia chama hiki;

“Kupitia nyie vijana wa Chama Cha Mapinduzi ambao leo hii ni viongozi wa UVCCM kuanzia ngazi ya wilaya,kata na mitaa kuhakikisha mnakisaidia chama hiki kinapata ushindi wa kishindo katika uchaguzi ujao wa 2019 wa serikali za mitaa ambapo ushindi wa kishindo wa CCM ndiyo utakaowezesha maandalizi ya ushindi wa kishindo wa uchaguzi mkuu wa 2020 hivyo jitoeni kwa hali na mali mkisaidie chama hiki,msikubali kuwa watumwa wa watu katika kuwachagulia viongozi tumieni akili zenu katika kujitafutia kipato halali ili muwe na jeuri kwa watu wanaotaka kuwaweka mifukoni” Alisema Makwiro

Aidha Mwenyekiti huyo amewasihi vijana hao kuwa na uvumilivu kusameheana kuondoa tofauti baina yao zilizopo ambazo zimetokana na uchaguzi wa ngazi mbalimbali za vijana wilayani humo kuwaomba waungane wakijenge chama kwa pamoja na kukivusha salama katika chaguzi zijazo za serikali ya mitaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Hata hivyo Mjumbe wa Baraza Kuu Taifa UVCCM Mkoa wa PwaniRamadhan Mlao amewakumbusha vijana wa mafia kushirikiana katika ngazi zote kuhakikisha wanaijenga jumuiya ya vijana kwa kushirikiana kwa pamoja kuanzia ngazi ya shina hadi wilaya ili wakisaidie chama katika chaguzi zijazo.

Akizungumza kwa niaba ya vijana hao,Mwenyekiti waUVCCM wa Wilaya ya Mafia,Amina Tuki,alisema kuwa wamepokea maelekezo kutoka kwa viongozi hao yeye akishirikiana na wajumbe wa baraza la vijana wa wilaya hiyo kuhakikisha wanaitisha mkutano ili kuondoa tofauti zilizopo ambazo zilisababishwa kwenye kipindi cha uchaguzi.

Lengo la ziara hiyo ni kuhakikisha kila mabaraza ya wilaya wanaelewa CBO kwa kina na ifanyiwe kazi kwa vijana kujiunga katika vikundi na kunufaika na fedha za vijana zinazotolewa na halmashauri husika ili kuinua uchumi wa vijana.

KIPINDI MAALUM KUAMSHA ARI YA WANANCHI KUSHIRIKI KATIKA SHIGHULI ZA MAENDELEO WILAYA YA KISARAWE PWANI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

DK. KIGWANGALLA AAGIZA JUMUIYA YA HIFADHI YA WANYAMAPORI WAMIMBIKI IPANDISHWE HADHI KUWA PORI LA AKIBA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Na Hamza Temba - WMU-Bagamoyo, Pwani
....................................................................

Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla amemuagiza Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, Maj. Gen. Gaudence Milanzi kuanzisha mchakato wa kisheria wa kupandisha hadhi Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori ya Wamimbiki kuwa Pori la Akiba ili iweze kuhifadhiwa vizuri baada ya kushindwa kujiendesha.

Ametoa agizo hilo leo mkoani Pwani baada ya kutembelea eneo la Jumuiya hiyo wakati wa ziara yake ya kikazi ya kukagua shughuli za uhifadhi katika eneo hilo ambalo ndani yake pia kuna mapito ya wanyamapori.

Dk. Kigwangalla amechukua uamuzi huo baada ya kutoridhishwa na utendaji kazi wa jumuiya hiyo ikiwemo tuhuma walinzi wake kutoka katika vijiji vinavyounda jumuiya kujihusisha na vitendo vya ujangili. Hata hivyo alipokea ombi la Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Omari Tofiki ambaye aliiomba Serikali ichukue jukumu la kulinda hifadhi hiyo kwa asilimia 100.

"Sisi kama jamii tumeshindwa, tunaomba msaada wa Serikali, itusaidie kuondoa hawa wavamizi na ikiwezekana ichukue jukumu la kulinda hifadhi hii kwa asilimia 100," alisema Tofiki.

Alisema jumuiya hiyo ambayo ni muunganiko wa vijiji 24 inakabiliwa na changomoto kubwa ya ujangili uliokithiri ambao umepelekea kuuwawa kwa wanyamapori zaidi ya asilimia 90 ya waliokuwepo tangu kuanzishwa kwa jumuiya hiyo mwaka 1997.

Alisema changamoto nyingine ni kukosekana kwa muwekezaji na mapato ya kujiendesha, uvamizi wa mifugo ndani ya hifadhi hiyo na majungu yanayosababishwa na baadhi ya wananchi na viongozi wanaonufaika na vitendo vya ujangili na uharibifu wa hifadhi hiyo.

Dk. Kigwangalla alisema jumuiya hiyo imefeli katika kila eneo jambo ambalo linalazimu kuanzishwa kwa mchakato wa kuirudisha Serikalini ili iweze kuhifadhiwa vizuri. Alitoa wito kwa viongozi wa Wilaya na vijiji kuanza kuwaelimisha wananchi juu ya umuhimu wa kupandishwa hadhi jumuiya hiyo kwa faida ya pande zote.

"Nimepokea maombi mengi ya kuongeza idadi ya wanyamapori katika hifadhi ya Saadan, tatizo kubwa hapa ni kwamba wanyamapori wanapotoka nje ya hifadhi hiyo na kupita kwenye eneo la Wamimbiki wanavunwa na majangili ambao wengi wao wanasuply (wanasambaza) nyamapori Jijini Dar es Salaam," alisema Dk. Kigwangalla akielezea umuhimu wa kupandishwa hadhi hifadhi hiyo.

Kwa upande wake Muwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania TAWA, Abraham Julu amesema Serikali imekuwa ikisaidia katika ulinzi wa eneo la jumuiya hiyo kwa kushiriki kwenye doria mbalimbali ambazo kwa kiasi kikubwa zimesaidia kuondoa makazi ndani ya hifadhi hiyo.

Alisema eneo hilo ni muhimu sana kwa uhifadhi wa wanyamapori kwa kuwa ni moja ya eneo la mazalia ya wanyamapori na shoroba nne (mapito ya wanyamapori) zinazounganisha hifadhi ya Taifa ya Saadan, Mikumi na Pori la Akiba la Selous.

Katika hatua nyingine baada ya kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Saadan, Dk. Kigwangalla ameuagiza uongozi wa TANAPA kupitia hifadhi hiyo kwa kushirikiana na uongozi wa Wilaya ya Bagamoyo na vijiji kuweka utaratibu maalum utakaowawezesha wananchi kupita katika barabara zilizopo ndani ya hifadhi hiyo kwa ajili ya shughuli za kijamii ikiwemo kuwatengenezea vitambulisho maalum.

Ametoa agizo hilo kufuatia malalamiko yaliyowasilishwa kwake na Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete kuwa wananchi wake wanazuiliwa kutumia barabara hizo kwa madai ya kushiriki kwenye vitendo vya uharibifu wa hifadhi hiyo.


Amewataka pia viongozi wa hifadhi hiyo ya pekee barani Afrika ambayo ipo katika fukwe za bahari ya Hindi kuwa wabunifu zaidi kwa kuanzisha bidhaa mpya za utalii ikiwa ni pamoja na kutangaza fursa zilizopo. Alisema hifadhi hiyo ambayo ipo karibu na Jiji la Dar es Salaam na Tanga ni fursa nzuri kwa watalii kutumia ukaribu huo kuweza kuwaona wanyamapori mbalimbali wakiwemo Simba, Twiga na Tembo pamoja na utalii wa fukwe.
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akizungumza na uongozi wa Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Wamimbiki wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua migogoro ya hifadhi katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Jana. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Majid Mwanga.

 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akikagua eneo la Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Wamimbiki wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua migogoro ya hifadhi katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Jana. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akisalimiana na wafanyakazi wa Hifadhi ya Taifa ya Saadan wakati wa ziara yake ya kutatua migogoro ya hifadhi katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Jana. Kushoto ni Mkurugenzi wa Uhifadhi wa TANAPA, Martin Loibooki. 
Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mazingira ya Hifadhi ya Taifa ya Saadan na Mhifadhi Mkuu wa Hifadhi hiyo, Stephano Msumi wakati wa ziara yake ya siku moja ya kutatua migogoro ya hifadhi katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Jana. Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akimsikiliza Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete wakati wa ziara yake ya kutatua migogoro ya hifadhi kwenye Hifadhi ya Taifa ya Saadan katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Jana. Katikati ni Mkurugenzi wa Uhifadhi wa TANAPA, Martin Loibooki. 
 Waziri wa Maliasili na Utalii, Dk. Hamisi Kigwangalla akioneshwa mazingira ya fukwe ya Hifadhi ya Taifa ya Saadan na Mbunge wa Jimbo la Chalinze, Ridhiwan Kikwete wakati wa ziara yake ya kutatua migogoro ya hifadhi katika wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani Jana.
Picha ya pamoja

VULLU ACHANGIA MIFUKO YA SARUJI UJENZI NYUMBA YA MGANGA, ZAHANATI YA KIJIJI CHA KOMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
KAIMU mkurugenzi halmashauri ya Mkuranga, Mkoani Pwani,ambae pia ni afisa maendeleo ya jamii,Safina Msemo akimshukuru mbunge wa viti maalum Mkoani Pwani, Zainab Vullu (kushoto aliyesimama)kwa kuchangia baadhi ya mifuko ya saruji kati ya mifuko 70 na malumalu vipande 500 vilivyogharimu zaidi ya mil.1.6
MBUNGE wa viti maalum Mkoani Pwani, Zainab Vullu, akimkabidhi kaimu mkurugenzi halmashauri ya Mkuranga, Mkoani Pwani,ambae pia ni afisa maendeleo ya jamii,Safina Msemo (mwenye gauni la kitenge) baadhi ya mifuko ya saruji kati ya mifuko 70 na malumalu vipande 500 alivyochangia ambapo vimegharimu zaidi ya mil.1.6.Picha na Mwamvua Mwinyi
 
………………

Na Mwamvua Mwinyi,Mkuranga.

MBUNGE wa viti maalum Mkoani Pwani,Zainab Vullu amekabidhi msaada wa mifuko 70 ya saruji pamoja na malumalu vipande 500 ,vilivyogharimu sh .milioni 1.6 ,katika halmashauri ya Mkuranga.

Kati ya vifaa hivyo mifuko 50 ya saruji ni mchango katika ujenzi wa nyumba ya mganga zahanati ya Kijiji cha Koma na mifuko mingine 20 ujenzi wa nyumba ya mwalimu shule ya msingi Kisiju Pwani.

Vullu alielekeza ,Malumalu (tiles)zipelekwe shule ya msingi Kisiju Pwani,katika ujenzi wa vyoo lakini aliomba kipaombele kipewe kwenye vyoo vya wanafunzi wa kike ili kujihifadhi wakati wakiwa katika hedhi .Aidha alisema anahamasisha ujenzi wa nyumba ya mganga na aliwataka wadau wengine waunge mkono jitihada za serikali ,halmashauri ,mbunge wa Mkuranga Abdallah Ulega aliyechangia mifuko 100 ya saruji .

Hata hivyo,Vullu alisema kilichomgusa kuchangia pia ni ilani ya Chama Cha Mapinduzi inaelekeza kusimamia maisha na maslahi ya mtanzania .
“Kijiji cha Koma hakina zahanati ,kutokana na suala hilo niliona nguvu za Mbunge ,halmashauri na ndipo Jan 1 ,nikwenda kuona hali ilivyo ,nimeona nitoe fedha za mfukoni mwangu nichangie mifuko ya saruji ujenzi wa nyumba ya mganga .” 

“Vijiji vya huko ni kisiwa ,ukitaka kufika lazima ukitoka ngambo hii hadi nyingine utumie lisaa hadi limoja na zaidi ,wakazi hao wakihitaji huduma zaidi za kiafya inabidi wakimbilie hospital ya wilaya ya Mkuranga ambako ni umbali mrefu “alisema Vullu .

Vullu alisema suala la afya ni muhimu hivyo kuna kila sababu ya kukamilisha ujenzi huo wa zahanati na nyumba ya mganga ili wananchi waondokane na kero yakufuata huduma za afya mbali .

Nae kaimu mkurugenzi halmashauri ya Mkuranga, ambae pia ni afisa maendeleo ya jamii ,Safina Msemo alishukuru kupata mchango huo.
Safina alisema kwa niaba ya halmashauri, alisema vifaa hivyo vitasaidia kuongeza nguvu kwenye ujenzi huo .

Kwa upande wake ,mwalimu mkuu wa shule ya msingi Kisiju Pwani, mwl.Jofrey Mbwale ,alitoa shukrani zake na kusema shule hiyo bado inakabiliwa na uhaba wa nyumba za walimu sita .Alisema kuna walimu nane nyumba zilizopo ni mbili huku alieleza kuna mahitaji ya walimu 20 .
Mwl.Mbwale alieleza mahitaji katika matundu ya vyoo ni matundu 41 yaliyopo ni 20 .

MBUNGE WA CHALINZE ATAFUTA UTATUZI MGOGORO WA ARDHI KWAMDUMA NA HIFADHI YA UZIGUA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MIGOGORO ya ardhi ni miongoni mua vitu ambavyo vimekuwa vikirudisha sana maendeleo nyuma.

Mara nyingi migogoro hiyo husababisha kusimama kwa shughuli mbalimbali za amendes kama ujenzi na kubwa zaidi shughuli za kilimo kwa wananchi wa maeneo husika hasa maeneo ya vijijini amber hutegemea arch kwa kuzalisha chakula.

Chalinze ni moja ya Halmashauri za Wilaya ya Bagamoyo, Mkoa wa Pwani ambazo zinakabiliwa na migogoro kadhaa ya ardhi. 

Miongoni mwah migogoro hiyo ni ule uliopo katika Kijiji cha Kwamduma Kata ya Kibindu, amber ni baissa ya kijiji hicho na Hifadhi ya Uzigua.

Katika kutafuta utatuzi wa migogoro hiyo, Mbunge wa Chalinze, Ridhiwani Kikwete alitembelea kijiji cha Kwamduma ili kuona namna ya kutatua agogo huh wa muda mrefu vaina ya Kijiji na Hifadhi.

Ridhiwani alisema lingo la tiara hiyo ni kuangalia athari za migogoro ya arch Latina kijiji Nicholas na kuzitafutia ufumbuzi baina ya wananchi na hifadhi".

"Nimefanya Ziara katika kijiji cha Kwamduma, Kata ya Kibindu kuangalia Athari za Migogoro Baina ya Kijiji na Hifadhi ya Uzigua, katika ziara hiyo tumeona hitaji la kukaa chini na watu wa hifadhi na kujadili suala la mipaka inayotembea,"alisema Ridhiwani. 

Alisema kuwa wamekubaliana na Serikali kuingilia kati mgogoro huo na kuutafutia ufumbuzi wa haraka.

"nashukuru Serikali imekubali kuushughulikia mgogoro huu kwa baraka ndani ya kipindi kifupi, ili shughuli nyingine za maendeleo ziendelee,"alisema Ridhiwani.

UJENZI WA RELI YA STANDARD GAUGE WA AWAMU YA KWANZA KUTOKA DAR ES SALAAM HADI MOROGORO WAENDELEA KWA KASI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Muonekano wa leo wa tuta la kutandazia reli ya kisasa (Standard Gauge) katika eneo la Soga mkoa wa Pwani takriban kilomita 37 kutoka Pugu mkoa wa Dar es salaam ulivyo sasa, ikiwa ni hatua iliyofikiwa katika muendelezo wa ujenzi wa reli hiyo ulioanza  mwezi Desemba mwaka jana katika mradi unaotarajiwa kukamilika ndani ya miaka mitatu na utajengwa kwa awamu nne. 

Kampuni Hodhi ya rasilimali za reli nchini (RAHCO) ndiyo inatekeleza mradi huo kutoka Dar es salaam kwenda Isaka na Mwanza imegawanyika katika awamu ndogo nne ikiwemo Dar es salaam hadi Morogoro, Morogoro hadi Makutupora, Makutupora hadi Tabora na Tabora hadi Mwanza.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mtendaji wa RAHCO Injinia Masanja Kadogosa jumla ya makandarasi  wanne wanaendelea na kazi usiku na mchana ili kukamilisha  ujenzi wa reli hiyo yenye upana wa mita 1.345 na ambao utaruhusu treni kutembea kwa spidi ya kilomita 160 kwa saa. Mradi huu mkubwa unatarajiwa  kuchochea maendeleo katika sekta ya kilimo, biashara, madini na viwanda hususan maeneo ambapo reli hiyo itapita ikiwemo  nchi  jirani ya Rwanda ambayo imekubali kujenga aina hiyo ya reli toka Isaka hadi Kigali.
Mtandao mzima wa reli nchini unaotegemewa kujengwa kwa kiwango cha standard Gauge una jumla ya kilometa 2,561 ukitarajiwa kugharimu Dola za Marekani Bilioni 7.683.  

PICHA NA IKULU

MGALU ARIDHISHWA NA KASI YA MKANDARASI SENGEREMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Naibu Waziri Wa Nishati ,Subira Mgalu mwenye kitambaa chekundu kichwani ,akiwa ameambatana na mbunge wa jimbo la Bagamoyo.dk.Shukuru Kawambwa wa pili kushoto na wengine ni viongozi mbalimbali wa kijiji cha Kongo na kata ya Yombo wakati alipokwenda kutembelea maeneo yanayotekelezwa mradi wa umeme vijijini (REA )awamu ya III ,ambapo amejiridhisha na kasi anayoendelea nayo mkandarasi Sengerema.(picha na Mwamvua Mwinyi)
 Nguzo 60 za umeme zilizotelekezwa ndani ya miaka mitatu huko kijiji cha Visezi Kata ya Vigwaza pasipo kufanyiwa kazi ,jambo linaloelezwa ni uzembe uliofanywa na mkandarasi MBH aliyepewa kazi awamu ya pili ya mradi wa umeme vijijini (REA )ambapo ameitia hasara serikali na kuchelewesha huduma ya umeme kwa jamii(picha na Mwamvua Mwinyi)
Naibu Waziri Wa Nishati ,Subira Mgalu akizungumza na wananchi wa kijiji cha Visezi kata ya Vigwaza kuhusiana na masuala ya huduma ya umeme.
 Mbunge wa jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete akizungumza jambo kuhusiana na changamoto ya nishati ya umeme huko kijiji cha Visezi kata ya Vigwaza.

Na Mwamvua Mwinyi-Bagamoyo

NAIBU Waziri Wa Nishati Subira Mgalu, ameridhishwa na kasi na kazi anayoendelea nayo ,mkandarasi wa mradi wa umeme vijijini (REA) awamu ya III, Sengerema huko kijiji cha Kongo na kata ya Yombo wilaya ya Bagamoyo ,Mkoani Pwani.

Aidha amelitaka shirika la umeme (Tanesco) wilaya ya Bagamoyo, kukimbizana na wakati kwa kuwapa wananchi fomu za kujaza ili kupatiwa umeme wakati zoezi la kuweka nguzo likiendelea katika baadhi ya vijiji.

Aliyasema hayo wakati alipokwenda kutembelea kijiji cha Kongo ,kata ya Yombo na Visezi kata ya Vigwaza na kujiridhisha na kazi ya mradi huo inavyoendelea .Mgalu alisema mkandarasi huyo ameahidi kumaliza kazi hiyo mwanzoni mwa mwezi ujao na kwa uhakika anakwenda vizuri.

Alieleza kwasasa amekuta wanaendelea na kazi ya kusimamisha nguzo na maeneo mengine yanatarajiwa kutandaza nyaya ."Mkandarasi Sengerema yupo Mkoa wa Iringa na Pwani ,ameanza kazi vizuri na ndivyo tunavyohitaji ,tunaomba aendelee na kasi hii ili wananchi wapate huduma hii ya umeme haraka" alisisitiza Mgalu.

Naibu waziri huyo,alitoa tahadhali kwa wakandarasi wengine wa mradi wa REA kwenda na kasi inayotakiwa na serikali ya awamu ya tano,na atakaefanya kazi chini ya kiwango hatakuwa na masihala nae.

Pamoja na hayo ,alilitaka Shirika la Umeme (TANESCO) mkoani Pwani,kwenda kuhakiki nguzo 120 zilizotelekezwa chini miaka mitatu mfululizo,.kwenye vijiji hivyo ,ili kujua kama bado zinauwezo wa kutumiwa

Mgalu alisema, nguzo 60 zilizopo kijiji cha Visezi na nguzo nyingine 60 kijiji cha Kongo ,zilipelekwa na mkandarasi MBH kwa maelekezo ya umeme vijijini (REA)awamu ya II ,ambae alifanya uzembe .

Alieleza ,Tanesco ihakikishe inahakiki nguzo hizo bila kufanya ajizi kwani serikali ilishamlipa fedha mkandarasi huyo awamu iliyopita ,hivyo itakuwa ni hasara kubwa kuziacha nguzo hizo pasipo kuzifanyia kazi .Mgalu alisema mkandarasi huyo ,hatoshi na amechelewesha huduma ya umeme kwa wananchi na atachukuliwa hatua za kisheria ili iwe fundisho kwa wakandarasi wababaishaji na wazembe.

”Ninaomba zikaangaliwe kama zinawezekana kufanyiwa kazi ,zitumike katika maeneo ambayo zitafaa kupelekwa ,kuliko kuendelea kukaa chini na kusababisha maswali ’alisema.

Mgalu aliwaeleza wakazi wa Visezi kuwa kijiji hicho kinatarajia kupata umeme kupitia mradi wa umeme unaotekelezwa katika mkoa wa Pwani na baadhi ya maeneo jijini Dar es salaam ikiwemo Kigamboni (PERI-URBAN).

Nae mbunge wa jimbo la Chalinze ,Ridhiwani Kikwete ,alisema anaimani na wizara ya nishati na nia nzuri ya serikali kwa kupeleka umeme katika vitongoji vyote na hakuna kitongoji kitakachoachwa.

Alisema ,kijiji cha Visezi kimezungukwa na fursa za chama cha ushirika cha umwagiliaji,gesi,ukaribu wa bandari kavu ya Kwala ,hivyo kinapaswa kupatiwa huduma ya umeme ili kunufaika na kuinua uchumi wake.

Ridhiwani ,alieleza ni wajibu wa wakandrasi na Tanesco kufanya kazi inayotarajiwa na jamii ili kuwaletea maendeleo wanayoyategemea .Baadhi ya wananchi wa kijiji cha Kongo,waliipongeza serikali kwa kuwasogezea huduma ya umeme karibu na wanaamini maendeleo yataongezeka.

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa