Home » » WANANCHI KIBAHA WAWAGOMEA TANROADS

WANANCHI KIBAHA WAWAGOMEA TANROADS

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAKAZI wa Kata ya Pangani na Maili Moja katika Halmashauri ya Mji wa Kibaha, wamewazuia Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) kuweka mawe katika maeneo yao kabla hawajalipwa fidia.
Maeneo hayo yamemegwa kutokana na upanuzi wa barabara ya Tamco-Mapinga.
Diwani wa Maili Moja, Andrew Lugani, akiaambatana na Mwenyekiti wa Serikali ya Machinjioni, aliwaambia waandishi wa habari kuwa anashangazwa kuona Tanroads wanaweka mawe kabla ya kukamilisha taratibu za kulipa fidia.
Lugano alisema tathimini katika eneo hilo imeshafanyika na kinachosubiriwa kwa Tanroads ni kulipa fidia kwa wananchi hao.
Akizungumzia suala hilo, Meneja wa Tanroads Mkoa wa Pwani, Tumain Sarakikya, alisema suala lao linashughulikiwa na litafanyiwa kazi muda wowote kuanzia sasa.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa