Home » » Azam yanogesha usajili kwa kumwaga fedha

Azam yanogesha usajili kwa kumwaga fedha

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Harakati za usajili zimeongezewa nguvu baada ya Kampuni ya Azam Media kutoa Sh462 milioni  kwa ajili ya maandalizi ya klabu za Ligi Kuu Bara msimu ujao utakaoanza Agosti 23.
Kutoka kwa fedha hizo katika wakati huu ni ahueni kwa klabu nyingi hasa ndogo ambazo zimekuwa hazina fedha za usajili na hata za maandalizi yao.
Usajili wa wachezaji wengi makini mara nyingi hufanywa na klabu kubwa zikiwamo Yanga, Azam na Simba huku klabu ndogo kwa miaka mingi zikiwa za mwisho huku zikisajili wachezaji wa kawaida kutokana na kukosa fedha.
Dirisha la usajili wa Ligi Kuu Bara litafunguliwa Juni 15 na kwa wa mujibu wa Ofisa wa Bodi ya Ligi, Silas Mwakibinga alisema fedha hizo ni za awamu ya kwanza ya fedha zinazotolewa kwenye udhamini wa Azam Media ambapo kila timu inapata Sh25 milioni katika fedha za awamu ya kwanza.
Ofisa mtendaji mkuu wa Azam Media, Rhys Torrington alisema fedha hizo zimetolewa mapema ili kusaidia maandalizi ya klabu za Ligi Kuu kama ilivyokubaliwa kwenye mkataba wa miaka mitatu ulioanza msimu uliopita.
Chanzo;Mwananchi 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa