Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
UJANGILI katika Hifadhi ya Taifa Ruaha umepungua kutokana na operesheni mbalimbali zilizofanyika katika hifadhi hiyo.
Mhifadhi Mkuu wa Ruaha, Dk. Chris Timbuka, aliwaambia waandishi wa
habari waliotembelea hifadhi hiyo jana kuwa kwa mwaka jana waliuawa
tembo 234, lakini mwaka huu idadi imepungua na kufikia 86.
Alisema kupungua kwa uhalifu huo kunatokana na Operesheni Tokomeza
ambayo waliitumia kukamata silaha na wahalifu kwa asilimia 60.
Alisema msako huo ulifanyika ndani na nje ya hifadhi ambapo silaha
zilikamatwa na wengine kupelekwa mahakamani ambapo kesi zao bado
zinaendelea.
“Ingawa uhalifu umepungua, lakini hali bado hairidhishi, kuna madhara
kwa wanyama na jitihada zinaendelea kufanyika ikiwa ni pamoja na
wizara kuongeza askari wa doria, silaha na kuwashirikisha wananchi
katika ulinzi huo,” alisema Dk. Timbuka.
Alisema Ruaha yenye ukubwa wa kilometa za mraba 20,200 ni ya kwanza
kwa ukubwa Afrika mashariki na ina tembo wapatao 20,000 kuliko hifadhi
nyingine yeyote na imekuwa kivutio kikubwa.
Akizungumzia utalii katika hifadhi hiyo, alisema hali ni nzuri ingawa
inahitaji kutangazwa zaidi kama ilivyokuwa kwa Serengeti na hifadhi
nyingine.
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment