Home » » WANAKIJIJI CHA MAISHA PLUS WASHINDA NA CHEMSHA BONGO, MWISHO WA SIKU WAFURAHIA PILAU.

WANAKIJIJI CHA MAISHA PLUS WASHINDA NA CHEMSHA BONGO, MWISHO WA SIKU WAFURAHIA PILAU.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Asubuhi ya leo wanakijiji walikuwa na sura zilizojaa bashasha na kufurahia maisha ya kijijini hapo. Shughuli mbalimbali ziliendelea huku wengine wakifanya usafi, kubadilishana mawazo wa ,asuala mbalimbali ikiwemo ufugaji wa kuku kwani ni moja ya miradi inayoendeshwa katika kijiji cha Maisha Plus na wengine wakiuza maandazi kijijini hapo ili kujipatia riziki na kujikimu na mahitaji muhimu katika familia zao. 

Wakati muuza maandazi akiendelea kufanya biashara yakatokea mabishano ya nani anayeweza kula maandazi mengi zaidi na mabishano hayo yakadumu kwa muda kadhaa lakini mwisho wa siku ni muuza maandazi kufaidika zaidi kwa kuwa aliweza kuuza kwa wingi.  


Baada ya hapo wanakijiji walipewa chemsha bongo na Masoud Ali, Mkurugenzi wa DMB na mwanzilishi wa Maisha Plus ambapo kila mwanakijijji alipata kipande cha picha ambacho kwa pamoja walitakiwa kuviunganisha na kupata picha mbili tofauti. 

Moja ya masharti ya chemsha bongo hiyo ni kuwa matatani kwa kundi la mwisho kufanikisha kuunganisha picha hizo na endapo zoezi hilo litashindikana basi kijijini hapo wasingeweza kuendelea na shughuli yoyote wala kula chakula cha usiku. Hivyo basi kila kundi lilijitahidi kuunganisha picha hizo kwa juhudi zote kwa kuhofia kuwa wa mwisho bila mafanikiwa kwa kuwa kundi la Maisha Plus lilikuwa na vipande vya picha mbili tofauti hali kadhalika na kundi la Mama Shujaa. 

Hivyo kundi moja lisingeweza kuunganisha na kupata picha moja iliyokamilika. Mara mwanakijini mmoja akaja na wazo la kuunganisha picha hizo kwa kushirikiana makundi yote mawili ndipo wakakubaliana na hoja hiyo hatimaye kufanikisha zoezi hilo. Hii inadhihirisha kuwa bila umoja na ushirikiano hakuna mafanikio yatakayoweza kupatikana katika jamii.

Makundi yote mawili walifurahi na kuweza kuendelea na shamra shamra za mapishi na walishirikiana kupika pilau na kula kwa pamoja kukamilisha furaha yao.

 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa