Home » » BAADA YA KUZIKOSA TSH.300,000 WANAKIJIJI WA MAISHA PLUS WAPATA MARKIA NA RAIS MPYA

BAADA YA KUZIKOSA TSH.300,000 WANAKIJIJI WA MAISHA PLUS WAPATA MARKIA NA RAIS MPYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


Kijiji cha Maisha Plus chapata Rais mpya ambaye huchaguliwa kila wiki. Huu ni utaratibu waliojiwekea wanakijiji cha Maisha Plus ambapo kila wiki hupata Rais mpya atakayeongoza kijiji hicho kwa kipindi cha wiki moja. Rais mpya wa wiki hii ni Mvano Ciza kutoka Burundi na mama yake ndiye aliyepotea katika mazingira ya kutatanisha kijijini hapo ambaye alitakiwa kuwa Malkia. Kwa sasa Rais amepata mama mwingine Mama Shujaa Upendo Msuya kutoka Kilimanjaro ambaye atakuwa Malkia kwa kipindi cha wiki moja na atakuwa mshauri na muamuzi wa masuala yote kijijini.
Baada ya uchaguzi wanakijiji waliendelea na shughuli zao za kawaida kama vile kupika, kufanya usafi na kutembeleana. Sambamba na hayo kijiji cha Maisha plus kilipata ugeni kutoka TAMASHA. Ugeni huo uliongozwa na Rukia Masayanyika Mratibu Mradi wa kuwafikia wasichana wadogo walio katika mazingira hatarishi nchini akiwa na watumbuizaji wa muziki kutoka Ujamaa Hip Hop Darasa ambao ni Nasri Kakiva, Calvin Samwel, Neyka Stanslaus na Khamisi Ramadhani.  Wanakijiji walipata darasa kupitia kisa mkasa walichotolewa na martibu wa TAMASHA uliochochea mjadala kuhusu ushiriki wa vijana katika masuala mbalimbali na kufanya maamuzi kwa manufaa yao wenyewe. Imeonekana kuwa vijana hufanyiwa maamuzi katika masuala yanayowagusa wao wenyewe inayopelekea vijana kuwa tegemezi hapo baadaye asijue nini cha kufanya kwa kuwa wameshazoea kupewa maelekezo kutoka kwa wazazi ama watu wanaowazidi umri. Kwa wanakijiji cha Maisha Plus mambo ni tofauti kwani vijana wapo mstari wa mbele katika nyanja zote ikiwemo uongozi, uchumi, utamaduni na kijamii kwa ujumla kwani tumeona vijana wakishika nafasi mbalimbali za uongozi tena za juu na kuleta mabadiliko kijijini hapo.
Kwa upande wa burudani Nasri Kaviva na Neyka Stanslaus walitoa burudani kwa wanakijiji cha Maisha Plus ambapo wanakijiji walifurahia sana burudani hiyo na kutaka kujua zaidi namna gani wanakijiji cha Maisha Plus wanaweza kuendeleza vipaji vyao ili nao waweze kufanikiwa katika siku za usoni ukizingatia kijijini hapo tayari kuna bendi ya Kantangaze ambapo wanaweza kuburudisha na kuonyesha vipaji vyao.
Pia siku ya leo wanakijiji walishiriki katika kinyang’anyiro cha fedha taslimu 300,000 kwa atakaye weza kuchukua ufunguo aliofungwa kwenye shingo ya chatu. Kila mwanakijiji alipewa sekunde tatu kufanya zoezi hilo la kuchukua ufunguo uliofungiwa shingoni mwa chatu kisha afungue boksi lililopo pembeni mwa chatu huyo ambapo ndani yake kulikuwa na fedha taslimu 300,000. Zoezi hili lilikuwa gumu kwa wanakijiji cha Maisha Plus kwani kuna ambao hawakuweza hata kumsogelea chatu huyo na wengine walijaribu kufanya hivyo lakini hawakufanikiwa kuchukua fedha zilizopo ndani ya boksi. Kutokana na muda uliowekwa kwa kila mwanakijiji hakuna aliyeweza kupata fedha hizo hivyo wanakijiji wamepoteza fursa hiyo ya kujipatia fedha hizo ambazo zingewasaidia katika kendeleza miradi yao hapo kijijini.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa