Home » » DARAJA LA MPIJI LAANZA KUPITIKA

DARAJA LA MPIJI LAANZA KUPITIKA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
John Pombe Magufuli
 
Daraja la Mpiji, Manispaa ya Kinondoni,  linalounganisha mkoa wa Dar es Salaam na Bagamoyo mkoani Pwani, limeanza kupitika baada ya ukarabati wa kipande kilichozolewa na maji kutengenezwa.
Magari yalianza kutumia barabara hiyo juzi usiku baada ya Wakala wa Barabara Tanzania (Tanroads) mkoani Dar es Salaam kutengeneza kipande kilichokuwa kimekatika.

Mhandisi wa Tanroads Dar es Salaam anayesimamia ujenzi huo, Ngusa Julius, aliwaambia waandishi wa habari waliotembelea daraja hilo kujionea maendeleo ya barabara hiyo, alisema hadi sasa eneo hilo limepokea malori 500 ya mawe na wanaendelea kujaza kwa kuwa yanatakiwa malori 700 ya mawe makubwa.

"Kwa sasa linapitika kwa upande mmoja hivyo magari yanapita kwa kupokezana, naamini hadi kesho kazi ya kujaza mawe na kusawazisha itakuwa imekamilika magari yatapishana bila wasiwasi," alisema.

Hata hivyo, Julius aliwataka madereva na watumiaji wengine wa barabara hiyo kuwa makini kwa kuwa kingo za barabara hazipo na kuna kina kirefu, hivyo ni rahisi kwa gari kuteleza na kutumbukia mtoni.

Daraja hilo lilikatika Aprili 13, mwaka huu kutokana na mvua kubwa iliyonyesha sehemu mbalimbali kwa siku mbili mfululizo.
SOURCE: NIPASHE

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa