Home » » Watakiwa kutekeleza mfumo wa stakabadhi

Watakiwa kutekeleza mfumo wa stakabadhi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MAOFISA Ushirika nchini kote wameagizwa kuhakikisha wanatekeleza mfumo wa stakabadhi ghalani ili kuimarisha vyama vya Ushirika nchini.
Rai hiyo imetolewa juzi wilayani Bagamoyo, Mgurugenzi na Mrajisi wa Ushirika nchini, Dkt. Audax Rutabanzibwa alipokuwa akizungumza na maofisa ushirika wa mikoa na wilaya mbalimbali nchini.
 Alisema kumekuwa na changamoto ya vyama vya ushirika kuchukua mikopo katika benki na kulipa wakati sio lengo la ushirika. Ushirika ni kukusanya na kutafuta soko kwa pamoja.
"Ushirika kazi yake n i kukusanya na kutafuta soko na sio wafanyabiashara, ushirika ukikopa unajiingiza kwenye deni ambalo analipa mwanachama,î alisema.
Aliendelea kueleza vyama vya ushirika vya msingi na vyama vya ushirika vikuu vinapaswa kuangalia upya kazi wanazofanya.
Aliviomba vyama vikuu visifanye kazi ya kukusanya badala yake wahusike kwenye ngazi za juu za mnyororo wa thamani wa zao, kama vile kutafuta soko la mazao ndani na nje ya nchi, kuogeza thamani kwenye mazao.
Alisisitiza kuwa kazi ya kukusanya waviachie vyama vya ushirika vya msingi ili kuepuka kuingiliana katika kazi na kuongeza gharama kwenye mnyororo wa thamani.
Semina hiyo iliyoandaliwa na Programu ya Miundombinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF) ililenga katika kuwaandaa maofisa ushirika nchini kuhusika zaidi katika kusimamia vyama vya ushirika vitekeleze Mfumo wa Stakabadhi ya Mazao Ghalani (Warehouse Receipt System) kupitia vyama vya ushirika.
Akizungumza katika semina hiyo mtaalamu wa masoko ya kilimo kutoka MIVARF, Muhoni Leonard alieleza kuwa kumekuwa na changamoto katika kuhusisha vyama vya ushirika visaidie wanachama kupata masoko ya mazao ya wanachama wao, lakini kwa kushirikiana na Tume ya Maendeleo ya Ushirika na wakulima wa chini zitakwisha.

Chanzo;Majira


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa