Home » » wahalifu waliotoka magerezani wawaumiza polisi pwani

wahalifu waliotoka magerezani wawaumiza polisi pwani

BAADHI ya vijana wahalifu waliotoka katika magerezani mbalimbali hivi karibuni ambao kesi zao zimeisha wamebainika kuwa washawishi wakuu na wanaoshirikiana na wahalifu na vibaka wengine kufanya matukio ya ujambazi na wizi wa mifukoni kwenye vituo vya mabasi huko mkoani Pwani. Akizungumzia matukio ya uhalifu sambamba na namna ya kukabiliana nao msimu huu wa siku kuu,Kamanda wa Polisi Pwani Ulrich Matei amesema mbali na kundi hilo pia limeibuka kundi jingine la watu ambao wanatumia fukwe ya Bahari wilayani Bagamoyo kama njia ya panya ya kupitisha madawa ya kulevya . Matei amesema jeshi hilo limeongeza nguvu na mbinu mpya ya kukabiliana na hali hiyo ambapo kwa kipindi cha wiki mbili zilizopita tayari wamewakamata wahalifu 43 waliotenda vitendo mbalimbali vya uhalifu huku kati yao vijana waliotoka gerezani hivi karibun baada ya kesi zao kuisha wakiwa ni zaidi ya 10. Amesema wahalifu hao kwa pamoja wanakabiliwa na makosa ya kukutwa wakisafirisha magunia saba za bangi na dawa za kulevya aina ya heroine na kokein pamoja na marobota 191 ya milungi Kamanda huyo amewaasa wananchi kushirikiana na jeshi hilo kutoa taarifa mara wanapogundua kuna watu wanaowatilia shaka na siyo kusubiri hadi wafanya uhalifu ndiyo wawatafute askari.
Katika hatua ingine magari zaidi 400 yamekamatwa kwa makosa mbalimbali ya barabarani katika operesheni maalumu ya kudhibiti madereva wazembe na wasiofuata sheria za usalama barabarani mkoani humo.
Matei ametaja makosa hayo ni pamoja na baadhi ya madereva kutumia vileo wakati wakiendesha,magari mabovu 151,mwendo kasi 67, yanayozidisha abiria 43 na yenye kupaki maeneo yasiyoruhisiwa 58.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa