Home » » RC PWANI WAKUWACHONGEA KWA JK WATENDAJI, WANASIASA WAZEMBE

RC PWANI WAKUWACHONGEA KWA JK WATENDAJI, WANASIASA WAZEMBE

MKUU wa mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza amesema hata sita kuwachongea moja kwa moja kwa rais Jakaya Kikwete viongozi na watendaji wa chama na Serikali wanaoendelea kuwa kikwazo cha maendeleo ya mkoa huo.

Mahiza alisema hayo leo wakati akizungumza na viongozi wa ngazi mbalimbali kutoka wilayani zote sita za mkoa huo waliohudhuria kikao cha kamati ya ushauri ya mkoa huo (RCC).

 Amesema ubunifu kwa mtumishi yeyote yule ni kitu muhimu zaidi katika utendaji kazi na siyo kufanya kazi kwa mazoea hivyo ni lazima kila mmoja kupitia fani yake na dhamana aliyopewa na Serikali abadili tabia  ili kukuza pato la uchumi la mkoa huo.

Mkuu huyo wa mkoa amesema wapo baadhi ya watendaji wamekuwa mzigo katika kutekeleza mikakati ya mkoa huo katika sekta za kilimo na uwekezaji hali ambayo imekuwa ikisababisha mkoa huo kutokuendelea kwa maana ya uchumi kubaki chini na pia fursa za wawekezaji kutotumika ipasavyo kutokana na ubunifu mbovu wa kiutendaji.

Amesema katika suala la kilimo wilaya zimekuwa ziking’ang’ana kuhamsisha kilimo cha korosho huku watendaji na hata wanasiasa wakijua ni zao la kudumu tena la enzi za ukoloni ambalo kila mzaliwa wa mkoa huo analijua umuhimu wake lazima atalilima tu kama mwana Pwani hivyo walipaswa kuhamsisha walime na mazao mengine ya muda mfupi kwani ardhi inaruhusu.

Mkuu huyo wa mkoa wa Pwani ameongeza kuwa yapo mazao mengine ya muda mfupi yenye masoko kama Ufuta,alizeti,mihogo na mahindi ambayo kama watendaji na wana siasa watawajibika kuhamasisha watu walime ni wazi kila mkazi atapata fedha za kujikimu kwa chakula,karo za shule, matibabu na dharura zingine za kifamilia huku wakisubiri zile za msimu wa korosho.

 Akizungumzia suala la mkoa huo kukosa maendeleo kupitia fursa za uwekezaji, Mahiza alisema ni kwa sababu bado baadhi wa viongozi ma wilayani  hawajawa wepesi wa kuruhusu ardhi itumike na wadau hao kwani wakitoa tu muda mfupi baadae huanzisha maandamano kupinga shughuli kuanza kwa kile wanachodai fidia.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa