Home » » Ajali 1,400 zaripotiwa Pwani

Ajali 1,400 zaripotiwa Pwani

JUMLA ya ajali 1,452 zimeripotiwa kutoka mkoani Pwani katika kipindi cha mwaka 2013 huku zilizosababisha vifo ni 240.
Akitoa taarifa ya mwaka, Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Ulrich Matei, alisema katika ajali hizo watu waliofariki dunia ni 314 na majeruhi ni 1,680.
Alisema Jeshi hilo pia limeweza kukusanya sh bilioni 1.6 kutokana na makosa 62,144 yaliyoripotiwa kwenye vituo vya polisi.
Kamanda Matei alisema kuwa katika makosa hayo, 61,032 yalilipiwa tozo na 1,112 madereva wake walipewa onyo.
Katika hatua nyingine, Kamanda Matei ametoa wito kwa wakazi wa Mkoa wa Pwani kuepuka kukaa katika maeneo ya ufukweni katika kipindi hiki cha sikukuu.
Alisema katika kipindi hiki kumeelezwa kuwepo kwa upepo mkali katika maeneo ya baharini, hivyo ni vema wananchi wakaepuka kukaa katika maeneo hayo.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa