Pwani. Mkoa wa Pwani unakabiliwa na tatizo
kubwa la wanafunzi wa kidato cha pili wanaotakiwa kukariri darasa
kukimbia shule na baadhi ya wanaopangiwa kidato cha kwanza nao
kutoripoti kabisa shuleni.
Kwa mujibu wa takwimu za Idara ya Elimu Mkoa,
zinaonyesha kuwa katika kipindi cha mwaka jana, zaidi ya wanafunzi wa
kidato cha pili 2,000 walishindwa kuendelea na masomo baada ya kufeli na
kutakiwa kukariri darasa.
Aidha, kwa upande wa wanafunzi waliopangiwa
kidato cha kwanza mwaka jana huohuo, zaidi ya 2,600 hawakuripoti shule
walizopangiwa na baadhi yao haikujulikana sababu kufanya hivyo.
Hayo yamebainika katika kikao cha kupitia
uchambuzi wa matokeo ya darasa la saba, ambapo wadau wa mkutano huo
walionyesha kusikitishwa na hali hiyo ambayo wameeleza ikiongezeka kila
mwaka.
Wakilalamikia hali hiyo, Mkuu wa Wilaya ya
Mkuranga, Mecy Sila, Mbunge wa Jimbo la Kibiti Abdul Marombwa, Asha
Itelewe na Shangwe Twamala walisema idadi ya wanafunzi wa kidato cha
pili wanaokimbia shule baada ya kutakiwa kukariri darasa imekuwa
ikiongezeka mwaka hadi mwaka tangu utaratibu huo ulipoanza.
“Wajumbe, hali ya watoto wetu kukimbia shule hasa
kidato cha pili tunaichukuliaje, maana kundi kubwa linakimbia na wakuu
wa shule wakiulizwa kutofahamu,” alisema
Pia baadhi ya wajumbe walilalamikia utaratibu wa
usahihishaji mitihani ya kidato cha pili kuwa siyo mzuri kutokana na
mitihani kutolewa mapema.
Chanzo;Mwananchi
Chanzo;Mwananchi
0 comments:
Post a Comment