NGOMA za usiku, mila
zilizopitwa na wakati sanjali na uwepo wa mashuga mami na mashoga imeelezwa
kuwa ni moja wapo ya sababu zinazochangia kuongezeka kwa maambukizi ya virusi
vya Ukimwi wilayani Kibaha mkoani Pwani kutokana na njia hizo kutumiwa
kuwahonga fedha ama zawadi zingine vijana wa kike na kiume
Kwa mujibu wa takwimu
za idara ya Ukiwmi zilizopo hivi sasa mjini Kibaha ni kwamba kiwango cha
maambukizi kwa watu waliopata ushauri na kupima VVU mjini Kibaha kimepanda
kutoka asilimia 7 saba mwaka jana hadi asilimia 9.7 tisa pointi
saba mwaka huu idadi ambayo imetajwa ni kubwa kuongezeka kwa kipindi kifupi cha
mwaka mmoja.
Akizungumzia hali hiyo,Mratibu wa Ukimwi mjini Kibaha Siwema Cheru amesema idadi ya watu waliofika kwenye vituo mbalimbali vya afya na kupata ushauri kisha kupima kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Desemaba mwaka huu ni watu 6,850 kati yao waliokutwa na VVU ni 665 wanaume wakiwa ni 214 na wanawake 451 hivyo kufanya kiwango hicho kufikia asilimia 9.7. sawa na ongezeko la asilimia tatu ya mwaka jana.
Akizungumzia hali hiyo,Mratibu wa Ukimwi mjini Kibaha Siwema Cheru amesema idadi ya watu waliofika kwenye vituo mbalimbali vya afya na kupata ushauri kisha kupima kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Desemaba mwaka huu ni watu 6,850 kati yao waliokutwa na VVU ni 665 wanaume wakiwa ni 214 na wanawake 451 hivyo kufanya kiwango hicho kufikia asilimia 9.7. sawa na ongezeko la asilimia tatu ya mwaka jana.
Cheru amesema takwimu
hizo ni zile tu zilizoripotiwa katika vituo vya afya na kwamba kuna uwezekano
mkubwa wapo watu wengi wagonjwa wa VVU ambao hawajajitokeza bado kwenye
vituo hivyo kwa uoga ama kujinyanyapaa wenyewe na badala yake kuendelea
kujiuguza nyumbani kwa kutumia dawa za asili.
Amesema mbali ya
hayo,nyumba za wageni zimekuwa hazizingatii umuhimu wa kuweka mipira ya
kujikinga yaani kondoms na zinaruhusu hata wenye umri mdogo na wasio wanandoa
kutumia vyumba.
Mratibu huyo wa
Ukiwmi mjini Kibaha Cheru amewaasa watu walioanza dawa za kufubaza virusi vya
makali ya Ukimwi-(ARVS) kuacha kusitisha dozi na kuendekeza ngono ili kuepuka
sugu wa ugonjwa huo sambamba na kunyemelewa na magonjwa mbalimbali
yanayopelekea vifo.
Nae mkuu wa wilaya ya Kibaha ,Hajat Halima Kihemba amesema kuna kila sababu ya watu kujitambua na kushirikiana Serikali kupambana na maambukizi mapya ya VVU,kukomesha unyanyapaa kwa wanaoishi na Ukimwi na kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.
Nae mkuu wa wilaya ya Kibaha ,Hajat Halima Kihemba amesema kuna kila sababu ya watu kujitambua na kushirikiana Serikali kupambana na maambukizi mapya ya VVU,kukomesha unyanyapaa kwa wanaoishi na Ukimwi na kupunguza vifo vinavyotokana na ugonjwa huo.
0 comments:
Post a Comment