Home » » Mahiza awaonya wafugaji kuibiana

Mahiza awaonya wafugaji kuibiana

MKUU wa Mkoa wa  Pwani Mwantumu MahizaMKUU wa Mkoa wa Pwani Mwantumu Mahiza amewaonya wafugaji mkoani hapa kuwapatia vijana wao ng’ombe wawapeleke malishoni kutokana na kuwepo kwa  wimbi la kuibiana mifugo.
Mahiza alitoa wito huo juzi wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake.
Alisema kumezuka wimbi la kuibiana mifugo migogoro ambayo inaashiria uvunjifu wa amani ndani ya Mkoa huu.
Bila kuwataja wafugaji kuwa wanatoka katika jamii gani Mahiza alisema wafugaji kwa wafugaji wamekuwa wakiibiana mifugo ikiwa machungani na katika kukabiliana na jambo hilo wamekuwa wakitumia silaha za jadi kutaka kuanzisha mapigano.
Alisema ofisi yake imesaidia kutuliza vurugu ambazo zilitaka kuanza kufuatia wizi huo, ambapo aliwaonya wafugaji hao kuachana na tabia ya kuwaagiza watoto kwenda na ng’ombe machungani.
“Wafugaji wanapowatuma vijana wadogo kwenda machungani wawe waangalifu kwa kipindi hiki inatakiwa waende watu wakubwa kuchunga ng’ombe wakati vuguvugu hili la wizi wa ng’ombe likiwa ndio tumelizima ili tujue kama limekwisha wasiwaachie watoto kubaki na ng’ombe maporini,” alisema Mahiza.
Alitoa rai kwa wafugaji wanaojijua hawako kihalali mkoani hapa wasiendelee kuwepo na wale ambao wapo kihalali wahakikishe hawawakaribishi wafugaji wenzao ili kupunguza ongezeko la mifugo.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa