CHAMA cha Waandishi wa Habari za Sayansi (TASJA), kimewataka wakazi
wanaoishi eneo la Hifadhi ya Saadani, kuhifadhi mazingira ya Mbuga
hiyo ili iweze kuendelea kuwa historia hadi katika vizazi vijavyo.
Mwenyekiti wa Chama hicho, Gryson Mutembei, alitoa wito huo hivi
karibuni, wakati wa ziara ya chama hicho katika hifadhi hiyo iliyolenga
kujifunza mazingira na viumbe hai.
Katika ziara hiyo iliyowezeshwa na Shirika la Elimu, Sayansi na
Utamaduni la Umoja wa Mataifa (UNESCO) na kutanguliwa na semina ya siku
mbili, Mutembei alisema baada ya mafunzo wamegundua jinsi mazingira na
viumbe hai vinavyotegemeana, hivyo kama wakazi hao hawatatunza
mazingira, hata wanyama hawatakuwepo.
David Ramadhani ni mmoja wa wanachama wa TASJA, alisema hakujua kama
Tanzania ina vivutio vizuri kama Saadani ambayo ni mbuga pekee
inayokutanisha bahari na mto, jambo linalofanya watalii wengi kwenda
kuangalia.
Kutokana na hilo, Ramadhani alisema safari za waandishi ni muhimu
mara kwa mara katika vivutio hivyo kwa sababu wataweza kutumia kalamu
zao kuvitangaza na kuvifanya vijulikane dunia nzima.
Mhifadhi Idara ya Ulinzi, Ismail Omar, alisema wamekuwa wakianzisha
miradi mbalimbali kwa wananchi kama mbadala wa kutowinda wanyama kwa
ajili ya kitoweo.
Omar alisema kumekuwepo na mahusiano mazuri ya kupata ujirani mwema
na wananchi ikiwemo katika kushiriki shughuli mbalimbali za maendeleo
Chanzo;Tazania daima
0 comments:
Post a Comment