Home » » MAHIZA AVALIA NJUGA MIGOGORO YA MIPAKA BAGAMOYO

MAHIZA AVALIA NJUGA MIGOGORO YA MIPAKA BAGAMOYO


Katika hatua inayodhihirisha Mkuu waMkoa wa Pwani, BI.MWANTUM MAHIZA ameamua kuchukua hatua za makusudi katika kukabiliana na migogoro ya mara kwa mara kati ya wafugaji na wakulima katika eneo la CHAMAKWEZA na PINGO wilayani Bagamoyo mkoa wa Pwani amechukua uamuzi mgumu wa kutembea jiwe hadi jiwe la mpaka.

Ilimlazimu Mkuu huyo wa mkoa BI.MAHIZA kutembea takriban kilometa 13 akiambatana na maofisa ardhi kutoka idara ya ardhi Bagamoyo ili kutafuta mawe ya mpaka unaoonyesha jinsi eneo hilo lilivyogawanya, na Chamakweza kwa wafugaji na Pingo kwa wakulima.

BI.MAHIZA katika ziara hiyo ya kukagua mipaka ya vijiji hivyo ameshuhudia mwenyewe jinsi ya wananchi ambao hawana nia nzuri na juhudi mbalimbali za usuluhishi zilizofanywa awali kwa kung’oa mawe yanaonyesha mipaka ya vijiji hivyo viwili vilivyopo katika mgogoro huo kwa karibu miaka 20 sasa.

Mkuu huyo wa mkoa wa Pwani amesisitiza kuwa makubaliano ambayo yalifikiwa awali ya kuweka mipaka kutenganisha maeneo hayo kwa misingi ya ufugaji na ukulima yaheshimiwe na hasa ikizingatiwa kuwa wajumbe waliofanya maamuzi hayo wanatoka pande mbili zinazokinzana za wakulima na wafugaji.

BI.MAHIZA amewataka wananchi wa pande zote mbili yaani wakulima na wafugaji kujenga desturi ya kuheshimiana kwa manufaa ya ustawi wao na maendeleo ya vijiji husika.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa