Home » » Akamatwa na noti bandia za shilingi mil. 3

Akamatwa na noti bandia za shilingi mil. 3

MKAZI wa kitopeni Lushoto Mkoani Tanga Ibrahim Bakari maarufu kama Semkumba,(36) anashikiliwa na jeshi la Polisi mkoani Pwani kwa kosa la kukutwa na noti bandia 304 za shilingi elfu 10 zikiwa na namba tofauti zenye thamani ya mil. 3,040,000

Kamanda wa Polisi mkoani humo,Ulrich Matei amesema mtuhumiwa huyo amekamatwa jana majira ya jioni huko Chalinze wilayani Bgagamoyo wakati akijaribu kununua maji kwa kutumia noti moja wapo kati ya hizo kwa mfanyabiashara ndogo ndogo wa eneo hilo.

Amesema muuzaji wa maji huyo alipata mashaka juu ya uhalali wa noti hiyo na kutoa taarifa kwa askari waliokuwa jirani ambao walimfuta kijana huyo na kumkamata kisha kumfanyia upekuzi na kukuta noti zingine 304 zikiwa zimehifadhiwa kwenye bahasha tatu tofauti kwenye begi lake.

Kamanda huyo alisema utaratibu huo wa kutumia noti bandia ni hatarishi kwa uchumi wa nchi  na hata mtu mmoja mmoja na hivyo jitihada zaidi za kuwabaini wanaohusika na mtandao huo zinafanyika sambamba na kusaka mashine zinazozalisha fedha hizo feki.

Katika tukio jingine mkazi wa Kitonga Rufiji Hamis Omary maarufu Chinga (15) amefariki dunia baada ya kukamatwa na mamba kisha kuraruliwa sehemu mbalimbali za mwili ikiwemo kichwa,wakati akiteka maji kwenye mto Rufiji.

Matei amesema tukio hilo limetokea majira ya saa nane mchana jana na mwili wa marehemu umekutwa ukiwa baadhi ya viungo vimenyofolewa ikiwemo mkono na mguu wa kushoto na kutupwa umbali wa km 4 toka eneo la tukio ndani ya mto Rufiji na tayari maiti imefanyiwa uchunguzi wa daktari na kukabidhiwa kwa ndugu kwa mazishi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa