Home » » Waliofeli kidato cha pili wakutwa wakiendelea kidato cha tatu

Waliofeli kidato cha pili wakutwa wakiendelea kidato cha tatu



SERIKALI imeendelea kuwasisitizia Wazazi na wanafunzi mashuleni kuwa wanafunzi wote 136,000 waliofeli kidato cha pili mwaka jana na kutakiwa kurudia darasa hilo wanapaswa kufanya hivyo bila kushurutishwa na kwamba wasijidanganye kuwua watafanya mitihani ya kumaliz akidato cha nne mwakani kwani namba zao hazipo.

Pia  wanafunzi hao wasije wakarubuniwa na baadhi ya walimu wakuu wa Sekondari nchini kuwa licha ya kufeli kwao wanaweza kuendelea na kidato cha tatu mwaka huu kwani hawataweza kufanya mitihani ya Taifa ya kidato cha nne mwakani kama wanavyodhani kutokana na namba na majina yao tayari zimeondolewa katika orodha hiyo ya mwakani.

Tahadhari hiyo imetolewa jana na Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi Philipo Mulugo wakati akifungua mafunzo ya Waratibu Elimu kata Kitaifa yanayoendeshwa na Wakala wa Maendeleo ya Uongozi wa Elimu (ADEM) huko Wilayani Bagamoyo Mkoani Pwani.

Mulugo amesema ana taarifa ya kuwepo kwa baadhi ya wanafunzi kati ya hao 136,000 ambao wameshawishiwa na Wakuu wa shule pamoja na wazazi wao kadhaa kuendelea na kidato cha tatu kwa matumaini ya kuwa watafanya mitihani ya kumaliza kidato cha nne mwaka ujao imani ambayo Waziri huyo alisema itakuja kuwaliza baadae maana kundi hilo halina nafasi ya kuhitimu mwakani.

Kutokana na hali hiyo Naibu Waziri Mulugo amewaagiza Waratibu Elimu Kata nchini wafatilie mara moja wanafunzi wote wa kidao cha pili waliofeli kama wamekariri darasa hilo kama ilivyoagizwa na Wizara na endapo watawabaini waliokaidi na kuendelea kidato cha tatu mwaka huu  watoe taarifa mapema ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao na walimu waliohusika na udanganyifu huo,
Awali Afisa Taaluma wa Mkoa wa Daresalaam Benadeta Thomas amesema mafunzo hayo ya waratibu elimu kata Kitaifa yanaendeshwa katika mikoa 11 nchini na ni utekelezaji wa mpango wa maendeleo ya Elimu ya Sekondari ngazi za kata na kwamba mikoa hiyo ni Daresalaam, Mbeya, Morogoro,Mtwara,Kilimanjaro,Singida,Ruvuma,Arusha,Tabora, Mwanza na Tabora

Benadeta ameongeza kuwa waratibu elimu kata hao pamoja na majukumu mengine waliyonayo sasa wanaanza kuwajibika kusimamia na kufatilia kwa karibu utoaji wa elimu ya sekondari katika ngazi ya kata ikiwemo kufatilia matumizi ya fedha na vifaa vya kufundishia na kufatilia na shughuli za ujenzi na ukarabati wa miundombinu mashuleni.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa