Home » » PROF. ELISANTE AAGIZA KIWANDA CHA VIUADUDU KUJITANGAZA

PROF. ELISANTE AAGIZA KIWANDA CHA VIUADUDU KUJITANGAZA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Elisante Ole Gabriel akiongoza kikao alipokutana na uongozi wa kiwanda cha Uzalishaji wa Viuadudu (Tanzania Biotech Production Limited) katika ziara yake ya kikazi jana Wilayani Kibaha. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Bw. Ramson Mwilangali.
 Kaimu Meneja wa Kiwanda cha Kuzazilisha Viuadudu (Tanzania Biotech Production Limited) Bw. Samwel Mziray akiwasilisha taarifa ya utekelezaji ya kiwanda hicho wakati wa ziara  ya kikazi ya Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Elisante Ole Gabriel (kushoto) jana Wilayani Kibaha. Kulia ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji (Biashara na Uwekezaji) Prof. Joseph Rwegasira Bushweishaija.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Elisante Ole Gabriel Profesa Elisante Ole Gabriel akisikiliza maelezo kuhusu dawa za kuulia mazalia ya mbu toka kwa Meneja wa Uzalishaji katika kiwanda cha Uzalishaji wa Viuadudu (Tanzania Biotech Production Limited) Mhandisi Aggrey Ndunguru alipotembelea katika kiwanda hicho  jana Wilayani Kibaha. Katikati ni Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo anayeshughulikia Biashara na Uwekezaji Prof. Joseph Rwegasira Bushweishaija .
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Elisante Ole Gabriel akisoma maelezo katika chupa ndogo ya dawa za kuulia mazalia ya mbu alipotembelea kiwanda cha kuzalisha dawa hizo cha Tanzania Biotech Production Limited kilichopo Kibaha Mkoani Pwani jana. Kushoto ni Kaimu Mkurugenzi wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Ramson Mwilangali na  Mhandisi Aggrey Ndunguru.
 Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Elisante Ole Gabriel akifafanua jambo mbele ya Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji (Biashara na Uwekezaji) Prof. Joseph Rwegasira Bushweishaija na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Maendeleo la Taifa (NDC) Bw. Ramson Mwilangali wakati wa ziara yao katika kiwanda cha Uzalishaji wa Viuadudu (Tanzania Biotech Production Limited) jana Wilayani Kibaha mkoani Pwani.
  Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Elisante Ole Gabriel akikagua mitambo ya kuzalishia bacteria ambayo hutumika katika kiwanda cha Uzalishaji wa Viuadudu (Tanzania Biotech Production Limited) wakati wa ziara yake jana Wilayani Kibaha mkoani Pwani. Kushoto ni Meneja Uzalishaji wa kiwanda hicho Mhandisi Aggrey  Ndunguru.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji Profesa Elisante Ole Gabriel akiwa katika picha ya pamoja na uongozi wa kiwanda cha Uzalishaji wa Viuadudu (Tanzania Biotech Production Limited) mara baada ya kumaliza ziara yake jana Wilayani Kibaha mkoani Pwani. Prof. Elisante amefanya ziara hiyo ikiwa ni kujitambulisha na kutembelelea baadhi ya taasisi na miradi iliyo chini ya Wizara yake.
Picha na: Frank Shija - MAELEZO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa