Home » » NAIBU WAZIRI MIFUGO NA UVUVI ULEGA AAHIDI KUTATUA MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI MKURANGA

NAIBU WAZIRI MIFUGO NA UVUVI ULEGA AAHIDI KUTATUA MGOGORO WA WAKULIMA NA WAFUGAJI MKURANGA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akizungumza na wananchi wa kijiji cha Kiramba kata ya Nyamato wakati wa ziara yake katika jimbo la Mkuranga na kuwaahidi kushugulikia mgogoro wa wafugaji na wakulima.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akisalimiana na wazee wa Kijiji cha Bigwa wakati wa ziara yake katika jimbo la Mkuranga jana Mkoani Pwani.
 Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega akizungumza na wanakijiji wa Mkiu wakati wa ziara yake ya Jimbo la Mkuranga na kuzungumza na wananchi wa eneo hilo.
Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi akisalimiana na wanakijiji baada ya kuwasili kwenye ziara yake katika Jimbo la Mkuranga jana Mkoani Pwani.Picha na Emmanuel Massaka.

Na Zainab Nyamka, Globu ya Jamii.

NAIBU Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega amesema atahakikishia mgogoro wa wafugaji na wakulima katika Wilaya ya Mkuranga unamalizika kwa kufikia makubaliano yenye kuleta tija.

Alizungumza hayo wakati wa ziara yake katika vijiji vya Kiramba, Mkiu, Bigwa na Kilimahewa Kusini, Naibu Waziri ambaye pia ni mbunge wa Jimbo la Mkuranga amesema kuwa mgogoro baina ya wafugaji na wakulima upo siku nyingi ila kwa sasa anataka kuhakikisha analitatua kabla kufikia kuleta madhara kwa wananchi wa maeneo hayo.

Ulega amesema kuwa, tatizo la mgogoro wa Wafugaji na wakulima lipo siku nyingi hata kabla ya yeye kuteuliwa na amepita kwenye vijiji hivyo na ameendelea kuliona ila kwa ushirikiano baina yake na Halmashauri ya Manispaa ya Mkuranga watafanikiwa kutatua mgogoro huo ambao bado haujawa mkubwa sana.

"Tatizo hili lipo siku nyingi, na tunalifahamu na tumeshaliona ila wanakijiji leo wamenikumbusha tena, mimi pamoja na jopo langu la watu kutoka Halmashauri tumejipanga kuona tunalitatua kwani bado halijafikia kuwa donda ndugu," amesema Ulega.

Katika Kijiji cha Kiramba na Mkiu, baadhi ya wananchi walitoa malalamiko yao kwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi Abdallah Ulega kuwa wafugaji waliokubaliwa na kijiji kwa ajili ya kuleta mifugo yao kwa sasa imekuwa kero wakiingia mpaka mashambani na kuharibu mazao yao.

Wanakijiji hao wamelalamika kuwa wafugaji walioidhinishwa katika mkutano wa kijiji wamekaribisha na ndugu zao ambapo kinasababisha mifugo kuwa mingi sana na mingine kuletwa mpaka kwenye mashamba yao kwa ajili ya malisho.

Mbali na hilo Naibu Waziri aliweza kukutana na changamoto ya barabara ya kimanzichana kulekea Kiramba, Tipo na Mkonoge na kumuagiza Mkandarasi kutoka Manispaa ya Mkuranga na Meneja wa TARURA kuhakikisha tatizo hilo linamalizika kabla ya kuanza kwa kipindi cha masika mwakani.

Katika ziara hiyo, Naibu Waziri Ulega ametoa mifuko ya saruji kwa Kijiji cha Kiramba, Mkiu, Bigwa na Kilimahewa Kusini kwa ajili ya muendelezo wa maendeleo ya kijiji humo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa