Waziri
wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi ajikuta
akikesha ofisini kwake pamoja na wananchi takriban 189 wenye Matatizo na
Kero za ardhi.
Mhe.
Waziri ametumia takriban saa 20 kusikiliza kero za wananchi ambao
waligoma kuondoka ofisini kwake hadi kero zao zitakapopatiwa ufumbuzi.
Kazi hiyo ilianza majira ya saa 2 asubuhi hadi saa 9 usiku.
Hata hivyo wananchi walilazimika kulala Wizarani wakisubiri kuonana na Waziri kutokana na uwepo wa idadi kubwa ya wananchi hao.
Wananachi
wengi wenye matatizo na Kero za ardhi kutoka maeneo ya Bagamoyo,
Kibaha, Mkuranga, Kibiti na Dar es salaam kwa ujumla wametumia fursa hii
ya kipekee ya kuonana na Waziri mwenye dhamana ya Ardhi na kumuelezea
kero zao na hatimaye kupatiwa ufumbuzi papo hapo.
Wananchi
hao wamesifu hatua hii ya Waziri Lukuvi kukutana nao ana kwa ana na
kuzitatua kero zao za ardhi kwa kuwa haijawahi kutokea. Nae Bwana
Francis Kamara mkazi wa Ilala jijini Dar es salaam amemuomba Waziri
aweze kuwaajibisha watumishi ambao wanakwamisha jitihada zake hadi
kupelekea yeye kukutana na wananchi moja kwa moja.
Mwanzoni
mwa mwezi Juni 2017 Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe.
William Lukuvi alitoa Tangazo la kuwataka wakazi wa kanda ya Dar es
Salaam na Pwani ambao wangependa kumuona, wafike katika
ofisi yake ya kanda ya Dar es Salaam iliyopo ghorofa ya pili, jengo la
Wizara ya Ardhi – Magogoni, Kivukoni ili kujiandikisha majina yao,
anuani na namba zao za simu.
Aidha,
Mhe. Waziri atafanya ziara kama hii katika kanda nyingine mara baada ya
kukamilisha zoezi hilo katika Kanda ya Dar es Salaam na Pwani.
0 comments:
Post a Comment