Home » » Polisi wamsaka aliyechoma bweni Mlandizi

Polisi wamsaka aliyechoma bweni Mlandizi

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

POLISI mkoani Pwani inaendelea kumtafuta mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Rafsanjani iliyopo Soga tarafa ya Mlandizi wilayani Kibaha mkoani Pwani baada ya kuchoma bweni la wasichana la shule hiyo.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani Pwani, Bonaventura Mushongi, mwanafunzi huyo ambaye hakuweza kufahamika alichoma bweni liitwalo Umoja juzi saa 4:00 usiku.
Alisema hata hivyo, tukio hilo halikuwa na madhara kwa wanafunzi zaidi ya kuharibu mali zilizokuwa kwenye bweni hilo ambazo thamani yake haikuweza kufahamika mara moja.
“Tunaendelea kumfuatilia mwanafunzi huyo ili tuweze kumjua na kumchukulia hatua za kisheria. Hadi sasa bado hatujafanikiwa kumpata kwani aliandika kwenye sanduku la maoni juu ya dhamira yake hiyo mbaya ya kuchoma bweni,” alisema Mushongi.
Alisema wanaendelea kuzifanyia kazi taarifa hizo ili wambaini mwanafunzi huyo kwa hatua zaidi za kisheria. Kikosi cha Zimamoto mkoani humo, Polisi pamoja na wananchi walifanikiwa kuuzima moto huo hivyo kuzuia usilete madhara kwa wanafunzi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa