Home » » 'WAHUDUMU WA AFYA ACHENI UBAGUZI'

'WAHUDUMU WA AFYA ACHENI UBAGUZI'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 
WATUMISHI wa Huduma ya Afya watakaogundulika kutoa huduma za ubaguzi kwa wanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) taarifa zao zitafikishwa wizarani, ili waweze kuchukuliwa hatua.
Baadhi ya watumishi katika idara ya afya wamekuwa wakilalamikiwa na wanachama wa mfuko huo kutoa huduma kwa ubaguzi kwa kuwathamini zaidi wagonjwa wanaotoa fedha papo papo.
Akizungumza mjini Kibaha hivi karibuni, Meneja NHIF Mkoa wa Pwani, Andrew Mwilungu, alisema wamekuwa wakipokea malalamiko mengi kutoka kwa wanachama wao na kwa sasa wanayafanyia kazi kwa kuwawajibisha watumishi wenye tabia hiyo, kwani imekuwa ikichangia baadhi ya wananchi kushindwa kujiunga na mfuko huo.
Mwilungu alisema kwa sasa wananchi wamekuwa wakihamasishwa kujiunga na mfuko huo, hivyo wako kwenye mkakati wa kurekebisha mapungufu yaliyopo kwa watoa huduma hao ambao wanatakiwa kubadilika na kuwathamini wanachama wa mfuko huo.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa