Home » » RC MAHIZA AIANGUKIA TCRA

RC MAHIZA AIANGUKIA TCRA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MKUU wa Mkoa (RC) wa Pwani, Mwantumu Mahiza, ameiomba Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) kuwasiliana na wamiliki wa vyombo vya habari, hasa luninga, ili kuweka mkalimani wa lugha ya alama katika taarifa za habari na vipindi maalumu.
Mahiza alisema uwepo wa mkalimani utawapa fursa watu wenye ulemavu wa kusikia (viziwi) kuelewa na kufuatilia kinachotangazwa.
Akizungumza wakati wa semina ya siku moja iliyoandaliwa na TCRA wakiishirikisha Taasisi ya Maendeleo kwa Viziwi (TAMAVITA), alisema kukosekana kwa mkalimani ni changamoto kwa viziwi.
Kwa upande wao, washiriki kutoka wilaya za mkoani Pwani, waliomba pia kuwepo na mkalimani kwani wanakabiliana na changamoto hiyo, pia wanapotumia mitandao ya simu za mkononi.
Ofisa Mkuu Masuala ya Mawasiliano wa TCRA, Thadayo Ringo, alisema wamepokea maoni yao na kuahidi kuyafanyia kazi ili kundi hilo lipate fursa ya kujua kinachotangazwa na kupata habari sawa na wengine.
Chanzo;Tanznia Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa