Home » » UKOSEFU WA ELIMU KIKWAZO KWA WAKOPAJI

UKOSEFU WA ELIMU KIKWAZO KWA WAKOPAJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MFUMO wa baadhi ya taasisi za fedha kutoa mikopo bila elimu kwa wanaokopa ni moja ya vyanzo vinavyochangia wanaokopa kushindwa kutumia mikopo hiyo kwa malengo waliyokusudia.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Simka, Lucas Mwamfupa, alibainisha hayo wilayani hapa mwishoni mwa wiki alipozungumza na waandishi wa habari  na kusema elimu ya mara kwa mara kwa wanaochukua mikopo inasaidia kuwakumbusha lengo la fedha wanazochukua.
Mwamfupa alisema baadhi ya taasisi zinazotoa mikopo zimekua zikishindwa kutoa elimu kwa wafanyabiashara wakubwa na wadogo wanaochukua mikopo, hali inayosababisha wengi wao kushindwa kurejesha na kufikishwa kwenye vyombo vya sheria.
Mkurugenzi huyo alisema katika kampuni yake hakuwahi kupata tatizo la mteja wake kukimbia na fedha, kushindwa  kurejesha mikopo yao kwa wakati kutokana na utaratibu waliojiwekea wa kuwapa elimu mara kwa mara na pia kuwaelimisha kuhusiana na athari za mikopo kabla hawajachukua.
“Tumekuwa na utaratibu katika kampuni yetu, kwa kuwaelimisha wateja wetu athari za kukopa na hii imesaidia wanaokopa kutokimbia na fedha ama kushindwa kurejesha fedha wanazokopa” alisema.
Katika mji wa Mlandizi, kampuni hiyo imeanza kukopesha wajasiriamali 13, kwa kutoa sh milioni 26 ikiwa ni baada ya kuwapatia elimu ya awali kabla hawajakabidhiwa mikopo yao.
SIMKA ilianzishwa mwaka 2008,  na sasa ina wajasiriamali 700 ambao wamenufaika na mikopo ya zaidi ya shi bilioni 1.7 katika maeneo ya Mafia, Kibaha, Kisarawe na Bagamoyo kwa mkoa wa Pwani, mkoa wa Dar es Salam wilaya zote, Mbeya katika maeneo ya Rungwe na Kyela.
chanzo :Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa