Home » » 'SERIKALI ITOE ELIMU SARATANI YA KIZAZI'

'SERIKALI ITOE ELIMU SARATANI YA KIZAZI'

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

SERIKALI na wadau mbalimbali wameshauriwa kufanya kampeni za wazi katika kukabiliana na ugonjwa wa saratani ya shingo ya uzazi kwa wanawake.
Mratibu wa Kitengo cha Uchunguzi wa Saratani ya Shingo ya Uzazi kilichoko hospitali ya Tumbi, Dk Alphonce Moyo, alisema jana kuwa inatakiwa kuwekwa mipango mahususi ya kuhakikisha wanawake wanapata elimu sahihi juu ya ugonjwa huo, ili wajitokeze kufanyiwa uchunguzi.
Moyo alisema endapo wanawake watapata elimu watahamasika kujitokeza kwa ajili ya kufanyiwa uchunguzi ambao kwa asilimia 90 unasaidia kumaliza tatizo la saratani ya kizazi kwa wanawake.
Alisema serikali imeelekeza nguvu kubwa katika kupunguza vifo vya wanawake wakati wa kujifungua, hivyo ni busara sasa kuwepo mikakati ya kuwanusuru wanawake hao na saratani hiyo ambayo ni tatizo kubwa nchini.
Aidha, alisema tangu kitengo hicho kianzishwe mwaka 2011, wanawake 1500 wamechunguzwa na waliogundulika kuwa na saratani ya awali ni wanawake  zaidi ya 50 ambao walipatiwa matibabu ya awali.
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa