Home » » POLISI ALIYEUAWA ASAFIRISHWA,MGAMBO AFARIKI

POLISI ALIYEUAWA ASAFIRISHWA,MGAMBO AFARIKI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

WAKATI mwili wa askari polisi mwenye namba, D 9887 Koplo Joseph Ngonyani wa Kituo cha Polisi Mkamba, Wilaya ya Mkuranga, mkoani Pwani ukisafirishwa leo kwenda mkoani Songea baada ya kuuawa na watu ambao wanadhaniwa kuwa jambazi, majeruhi mmoja kati ya wawili Venance Francis ambaye ni mgambo, naye amefariki dunia.

Francis ambaye naye alijeruhiwa katika tukio hilo baada ya watu hao kuvamia kituo hicho cha polisi, kupola silaha na risasi, amefariki dunia jana katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam, wakati akiendelea kupatiwa matibabu.

Akizungumza na Majira jana, Bi. Annastazia Nyonyani ambaye marehemu Koplo Nyongani ni baba yake mdogo, alisema mwili huo umesafirishwa jana kwenda Songea, Kijiji cha Namasengo kwa mazishi.

"Tumeaga mwili saa sita mchana, saa nane tulianza safari ya kwenda Kijiji cha Namasengo kwa mazishi ambayo yatafanyika kesho (leo), kwa sasa bado tupo safarini," alisema.

Marehemu Koplo Ngonyani alifariki dunia akiwa njiani kupelekwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mkuruanga baada ya kukamtwa mapanga na watu hao ambao walivamia kituo hicho, kupora silaha mbili aina ya SMG.

Zilaha hizo, zote zikiwa na magazini mbili zenye risasi 30 kila mmoja na kuwajeruhi mgambo wawili waliokuwa kituoni hapo akiwemo marehemu Francis na mwenzake Mariam Mkamba.

Akizungumza na Majira, Msemaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Aminiel Eligaisha, alithibitisha kifo cha marehemu Francis na kuongeza kuwa, mwenzake Mkamba anaendelea na matibabu kwenye Kitengo cha Mifupa (MOI), kilichopo hospitalini hapo.

"Marehemu alifikishwa hospitalini hapa juzi akitokea hospitali ya Wilaya ya Mkuranga...amefariki leo (jana), saa nne asubuhi," alisema.

Taarifa zilizolifikia gazeti hili kutoka vuanzo mbalimbali, zinasema jeshi hilo linawashikilia baadhi ya watu wakihusishwa na tukio hilo na wanaendelea kuhojiwa.

Awali Kamanda wa Polisi mkoani humo, Ulrich Matei alisema jeshi hilo litahakikisha silaha zote zilizochukuliwa na watu hao zinapatikana haraka akiwataka wananchi kuwa wavumilivu kuhusiana na tukio hilo.

Kamishna Suleiman Kova

Katika hatua nyingine, Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, limeunda kikosi maalum cha upelelezi kwa kushirikiana na jeshi hilo mkoani ili kufuatilia tukio la mauaji ya polisi huyo na uporaji wa silaha.

Akizingumza na waandishi wa habari Dar es Salaam jana, kamanda wa kanda hiyo, Kamishna Suleiman Kova, alisema tukio hilo kikosi hicho kitafanya kazi usiku na mchana ili kuhakikisha silaha zilizoporwa zinapatikana na wahusika wanakamatwa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa