Home » » SUMATRA KUWABANA MADEREVA WAKOROFI

SUMATRA KUWABANA MADEREVA WAKOROFI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA), inatarajia kuanza utaratibu wa kutoa vibali maalumu vitakavyolenga kumuwajibisha dereva au kondakta moja kwa moja badala ya mmiliki kama ilivyokuwa awali, lengo likiwa ni kudhibiti makosa ya barabarani.
Ofisa Mkuu wa Sumatra Mkoa wa Pwani, Iroga Nashon, alieleza hayo juzi alipozungumza na waandishi wa habari. Kwamba mamlaka hiyo imefikia hatua hiyo baada ya baadhi ya madereva kurudia makosa mara kwa mara, hata baada ya kutozwa faini.
Alisema awali kosa lolote ilimbidi mmiliki kuwajibika ikiwemo kutozwa faini ambayo huanzia sh 250,000. Lakini kwa sasa itamlazimu dereva ama kondakta kuwajibishwa moja kwa moja ili kuwawezesha waheshimu sheria zilizowekwa.
Nashon alisema vibali hivyo pia vinalenga kuwarekebisha na endapo dereva au kondakta atakutwa na kosa atanyang’anywa kibali na kuzuiliwa kazi hadi atakapojirekebisha.
Alisema mpango huo wa kitaifa upo kwenye hatua za awali na unatarajiwa kuanza kutumika baada ya mwaka wa fedha ujao.
 Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa