Home » » MISS KIBAHA KURINDIMA KESHO

MISS KIBAHA KURINDIMA KESHO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
Washiriki Miss Kibaha 2014KINYANG’ANYIRO cha kumsaka mlimbwende wa Kibaha, Miss Kibaha 2014 kinatarajiwa kurindima katika Ukumbi wa Container mjini hapa kesho.

Akizungumza na Tanzania Daima, Mratibu wa shindano hilo, Teddy Chilala, alisema kwa sasa tayari warembo wanane wameshaanza kujinoa vilivyo katika Ukumbi wa Blue Nile na kuwa maandalizi yote yanakwenda vizuri.
Mratibu huyo alibainisha kuwa shindano hilo litapambwa na burudani mbalimbali za muziki wa dansi hapa nchini, ikiongozwa na bendi ya JKT Ruvu chini ya kiongozi wao mpya, Hamis Kayumbu ‘Amigolas’ pamoja na Mhina Panduka ‘Toto Tundu’.
Aliongeza kuwa shindano la mwaka huu litakuwa la aina yake, kutokana na kuwashirikisha warembo ambao ni wazawa wa Wilaya ya Kibaha na kutoa wito kwa wakazi wa mji huo na maeneo mengine ya jirani, kujitokeza kwa wingi kwenda kushuhudia onyesho hilo.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa