Home » » MWENYEKITI WA CCM ALIWA NA MAMBA RUFIJI

MWENYEKITI WA CCM ALIWA NA MAMBA RUFIJI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mwenyekiti wa CCM, Tawi la Lumumba katika Kijiji cha Kilimani Mashariki kilichopo Kata ya Ngorongo, Rufiji, Saidi Simba (60), amefariki dunia kwa kuliwa na mamba baada ya kuzama na mtumbwi alipokuwa akienda shambani.
Ofisa Mtendaji wa Kijiji cha Kilimani Mashariki, Masudi Mminge alisema tukio hilo lilitokea juzi katika Mto Rufiji wakati mwenyekiti huyo alipokuwa akivuka kwenda ng’ambo ya pili kwa ajili ya kilimo.
Mminge alisema jitihada za kumtafuta zimekwama kutokana na eneo hilo kuwa na mamba wakubwa hivyo kuwafanya wananchi kuwa na hofu ya kuliwa.
Alisema kila walipokuwa wakifika sehemu za vichaka vya mto walikuwa wakisikia harufu kali lakini juzi harufu hiyo ilitoweka jambo ambalo limewafanya waamini kuwa ndugu yao ameshakufa na ameliwa na mamba.
Chanzo:Mwananchi

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa