Home » » MAISHA PLUS/MAMA SHUJAA WA CHAKULA YAZIDI KUNOGA WANAKIJIJI CHA MAISHA PLUS WAPATA UJUZI ZAIDI.

MAISHA PLUS/MAMA SHUJAA WA CHAKULA YAZIDI KUNOGA WANAKIJIJI CHA MAISHA PLUS WAPATA UJUZI ZAIDI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 




Maisha ya wanakijiji cha Maisha Plus yameendelea kuwa mazuri siku hadi siku. Kazi ziliendelea kama kawaida huku wanakijiji wakijadili na kutafakari toka walipowasili kijijini hapo mpaka sasa. Wanakijiji wengi walikuwa na mtazamo tofauti walipoingia tu kijijini na kudhani kuwa watashughulika na kilimo pekee. Hali imekuwa tofauti kwani wanakijiji wameweza kujifunza mambo mbalimbali mazuri na yenye manufaa kwa mtu mmoja mmoja na jamii kwa ujumla punde watakapo rudi. Uzoefu walioupata mpaka sasa ni pamoja na utengenezaji wa batiki, sabuni ya maji na kibande, mafuta mazito ya kujipaka, utengenezaji wa jiko la gesi, jiko linalotunza joto, ufugaji bora wa kuku bila kusahau kilimo hai.
Pamoja na hayo baadhi ya vijana wa kijiji cha Maisha Plus kwa siku ya leo walikwenda porini kwa lengo la kuweka mitego ya kutega ndege aina ya kanga na samaki katika bwawa lililopo jirani na kijiji hicho. Vijana hawa wamefanya hivyo kama mchango wao kusaidia familia zao kupata kitoweo japo hawakuweza kupata chochote kwa siku hiyo na kurudi nyumbani mikono mitupu.
Kwa kuwa wanakijiji walikosa fursa ya kuchukua ufunguo uliopo kwa chatu na kufungua  boksi lililo na fedha taslimu kiasi cha shilingi 300,000 wanakijiji hao walipewa swali ambalo halikuweza kurudiwa na muulizaji na haikuruhusiwa kuuliza maswali kama masharti ya swali hilo ili kuwaachia wanakijiji hao kazi ya kutafakari na kufanya kile walichoagizwa. Swali hilo lilikuwa linasema hivi ‘tengeneza system yenye mfumo wa mchanganyiko wa hydrotherapy na liquid therapy bila kuhusisha maji kwa ajili ya kupunguza magonjwa ya kuharisha kwa watoto wadogo walio chini ya umri wa miaka mitano’ je, swali la kujiuliza wanakijiji cha Maisha Plus wataweza kutengua kitendawili hicho? Tuone kipindi kijacho kwani wanakijiji hicho walikuwa bado wanajadili nini cha kufanya.
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa