Home » » WANAOWAFICHA WALEMAVU WASHITAKIWE

WANAOWAFICHA WALEMAVU WASHITAKIWE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

SERIKALI mkoani Pwani imeombwa kuwachukulia hatua za kisheria wazazi wenye tabia ya kuwaficha watoto wenye ulemavu kwa kuwa kitendo hicho kinawanyima haki za msingi ikiwemo kusoma.
Wito huo ulitolewa juzi na Mke wa Mbunge wa Kibaha Mjini Sylivester Koka (CCM), Selina, alipozungumza na wazazi na watoto wenye ulemavu wakati wa ziara aliyoifanya kwenye kata za Wilaya ya Kibaha kwa lengo la kuwasaidia walemavu na wanaoishi kwenye mazingira magumu.
Selina alisema baadhi ya wazazi wilayani humo wanawaficha ndani watoto wenye ulemavu hali inayowakosesha haki na mahitaji yao muhimu.
Alisema jamii ya wenye ulemavu nayo ina haki sawa na wengine, hivyo ni vema serikali kuwawajibisha wazazi wenye tabia hizo ili kuwa fundisho kwa wengine na kuondoa unyanyapaa katika jamii.
Mke wa mwanasiasa huyo aliwasaidia watoto yatima, walemavu na waishio kwenye mazingira magumu wapatao 100, vyakula mbalimbali, vifaa vya shule na sabuni, mali zenye thamani ya sh milioni tano.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa