Home » » HOSPITALI TUMBI YAHITAJI KITUO CHA DAMU SALAMA

HOSPITALI TUMBI YAHITAJI KITUO CHA DAMU SALAMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Hospitali Tumbi yahitaji kituo cha damu salamaHOSPITALI Teule ya Rufaa ya Tumbi iliyopo Kibaha mkoani Pwani, inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa kituo cha damu salama.
Ukosefu wa kituo hicho umekuwa ukisababisha damu inayokusanywa hospitalini hapo kutotumika hadi pale itakapopelekwa makao makuu ya damu salama kupimwa na baadae kugawanywa kwenye hospitali na vituo vya afya.
Akizungumza na waandishi wa habari waliotembelea hospitali hiyo kujua changamoto zinazoikabili, Kaimu Mganga Mkuu wa hospitali hiyo, Dk. Brayson Kiwelu, aliomba wafadhili kujitokeza kusaidia ujenzi wa kituo hicho, ili damu inayokusanywa iweze kutumika kwa wagonjwa wa hospitali hiyo.
Alisema endapo kituo hicho kitajengwa kitasaidia kuondoa upungufu wa damu katika hospitali hiyo pamoja na watu wengi kujitokeza kuchangia damu.
“Hospitali yetu imekuwa ikikusanya damu nyingi, lakini kutokana na kutokuwa na kituo damu hiyo imekuwa ikienda kupimwa makao makuu na baadae tunapata mgawo kama hospitali nyingine ambao damu hiyo haikidhi,” alisema Dk. Kiwelu.
Hospitali hiyo pia inakabiliwa na upungufu wa madaktari ambapo kwa sasa wapo 11 huku wanne kati yao wakiwa masomoni.
Pia Dk. Kiwelu ameiomba serikali kusaidia fedha kwa ajili ya ukarabati wa majengo ya hospitali hiyo kutokana na mengi kuchakaa.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa