Home » » BAGAMOYO WANYWA MAJI YA MALAMBO

BAGAMOYO WANYWA MAJI YA MALAMBO

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
WAKAZI wa Kijiji cha Dihozile, Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani, wanatembea kwa saa mbili kufuata huduma ya maji ya malambo.
Wakizungumza na Tanzania Daima hivi karibuni, walisema tangu kijiji hicho kianzishwe hawajawahi kupata huduma ya maji, hivyo kulazimika kutumia maji ya malambo.
Mwajuma Hamis, mkazi wa Dihozile, aliiomba serikali kuingilia kati kusaidia upatikanaji wa maji katika kijiji chao ili kuondokana na adha ya kutumia muda mwingi kufuata huduma hiyo.
Mwajuma alisema baadhi ya shughuli za kimaendeleo zinashindwa kufanyika kwa wakati kutokana na ukosefu wa maji ya uhakika katika eneo hilo.
Nao wakazi wa Kijiji cha Saadani Chumvi wilayani hapa, wanakabiliwa na changamoto ya ukosefu wa maji safi na salama, na hivyo kulazimika kutumia maji ya malambo ambayo hutumiwa pia na wanyama waliopo kwenye hifadhi.
Hadija Juma, mkazi wa kijiji hicho, ameiomba serikali kuwasaidia kuwafikishia huduma ya maji katika eneo lao kwani kwa sasa wako katika hali mbaya ya kutumia maji na wanyama ambayo yamekuwa yakiwasababishia homa za matumbo.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa