Home » » Mbaroni kwa kujifanya askari Polisi

Mbaroni kwa kujifanya askari Polisi

JESHI la polisi mkoani Pwani linamshikilia Daud Ramadhani (21) kwa kosa la kujifanya askari polisi.
Mtuhumiwa huyo alikamatwa Disemba 29 saa nne usiku katika eneo la Kwamatiasi kata ya Mkuza wilaya ya Kibaha mkoani Pwani, baada ya jeshi la Polisi kupata taarifa kutoka kwa wananchi zilizodai kuwepo kwa mtu anayejifanya askari.
Kamanda wa Polisi mkoani Pwani Ulricha Matei alisema baada ya kupata taarifa hizo waliandaa mtego ambao juzi wakafanikiwa kumkamata mtuhumiwa huyo akiwa na kitambulisho bandia cha polisi, jozi moja ya sare polisi jozi tatu za viatu vya Polisi.
Vitu vingine alivyokutwa navyo kwa ajili ya shughuli zake za kipolisi ni pamoja na mikanda miwili ya kiunoni, kofia moja aina ya Balet pamoja na mkanda wa filimbi.
Matei aliongeza kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa na kitambulisho chenye namba H,136,2 Police kikiwa na majina ya Daud Ramadhani Iddi.
Alisema uchunguzi unaendelea na mtuhumiwa atafikishwa mahakamani upelelezi utakapokamilika
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa