Home » » Wasisitiza elimu ya uzazi shuleni

Wasisitiza elimu ya uzazi shuleni

WATOTO wengi walio shuleni hawana elimu ya uzazi hali inayochangia ongezeko la mimba shuleni.
Mwenyekiti wa shirika lisilo la kiserikali la Tanzania Pre mature Mothers Organization (TPMO), Konsolata Kayaga, alisema hayo mjini hapa jana na kuongeza kuwa wameamua kutoa elimu ya mimba za utotoni ili kupunguza tatizo hilo ambalo linachangia kudumaza maendeleo kwa ajamii.
Kayaga alisema kwa sasa wameanza kutoa elimu hiyo kwa watoto yatima wa kituo cha Buloma kilichoko Kibaha, Pwani, ili kuwasaidia kujikinga na maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU) pamoja na mimba za utotoni.
Alisema lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha watoto hususan wa kike kutambua kuwa mimba za utotoni ni hatari kwa maisha yao, kwani mara nyingi zimekuwa zikisababisha vifo.
Alisema ili kuweza kufikia malengo ni vema jamii ikashirikiana kupiga vita mimba za utotoni ambapo kufanya hivyo kutakuwa njia sahihi ya kuokoa maisha ya watoto wa kike.
Ofisa Tarafa wa Wilaya ya Kibaha, Anatory Mhango, alivitaka vituo vya kulelea watoto yatima kuhakikisha vinatoa elimu na maadili mazuri kwa watoto hao, ili waweze kupunguza uhalifu na hatimaye waepuke vishawishi vya wanaume wakiwa shuleni.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa