VIONGOZI wengi
wakiwamo wabunge na mawaziri nchini imeelezwa wamekuwa wakipata ugonjwa wa
kiharusi na hatimaye kupooza na kupoteza maisha muda mfupi toka wanapokuwa
wametoka madarakani kutokana na kufanya vitendo vya udanganyifu wakati wa
kujaza fomu za tume ya maadili na utumishi wa umma.
Udanganyifu huo
umekuwa ukifanywa na viongozi wengi ambapo badala ya kuweka wazi mali zao,wao
huamua kuwaandikisha ndugu au jamaa zao katika mali na miradi na kutokana na
kutokuwa waaminifu ndugu ama jamaa hao huamua kuwadhulumu hivyo viongozi hao
wanaporudi mtaani hupatwa na matatizo hayo baada ya kushtushwa na hali
wanayoikuta katika miradi yao.
Hayo yameelezwa leo
Nov 5 wilayani Kisarawe na Afisa kutoka Sekretarieti ya maadili ya utumishi wa
umma, Zahra Guga kwenye uzinduzi wa mradi wa kutumia misingi ya utawala bora
katika kupambana na mabadiliko ya tabia nchi
Uzinduzi wa mradi huo
umefanyika katika kata za Chole na umelenga kutekelezwa kwenye kata tatu
ikiwemo Vikumbulu na Marui wilayani Kisarawe na asasi isiyo ya kiserikali ya
Guluka-Kwalala chini ya ufadhili wa shirika lisilo la kiserikali la The
Foundation for Civil Socieyt kwa sh. milioni 135 kwa miaka 3.
Ameongeza kuwa
hata wabunge na wengineo wanapata stroke kwa sababu wanapomaliza uongozi na
kurudi kule katika miradi anakuta mambo aidha ni mabaya sana kwa maana
umefilisika au mtu aliyemkabidhi ameamua kumdhulumu hivyo kubaki anang’aa macho
hana pa kukimbilia.
Guga amesema inawawia
vigumu kumsaidi mbunge,Waziri au kiongozi wa namna hiyo kwa sababu yeye anakuwa
amemkabidhi mali au mradi ndugu au jamaa yake kwa maandishi kabisa na hivyo
kukosa umiliki halali.
Aidha Afisa huyo
kutoka tume ya maadili ya watumishi wa Umma,amesema tatizo kubwa ambalo tume
hiyo imekuwa ikikumbana nalo kwa sasa ni kutokuwapo kwa mifumo
madhubuti,migongano ya maslahi,uwezo wa taasisi simamizi za maadili kifedha na
rasilimali watu na mmonyoko wa maandili miongoni mwa jamii.
Kauli hiyo ya Tume ya
Maadili na utumishi wa umma inakuja huku ikiwa ni siku chache tu tokea Spika wa
bunge la Jamhuri ya Muungano Anna Makinda kueleza kukerwa na baadhi ya
Wabunge wa zamani ambao wamekuwa wakifika katika ofisi yake na kulia wakiomba
kusaidiwa kutokana na kukabiliwa na maisha magumu.
0 comments:
Post a Comment