Home » » PAC yasema lazima vyama vikaguliwe

PAC yasema lazima vyama vikaguliwe



MAKAMU Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), Deo Filikunjombe, amesema ni lazima vyama vya siasa vifanyiwe ukaguzi kwa kuwa vinapokea fedha za umma.
Hayo aliyasema juzi wakati wa ufunguzi wa mafunzo kwa wajumbe wa Kamati ya PAC na ile ya Serikali za Mitaa (LAAC) iliyofanyika Bagamoyo, Pwani.
Filikunjombe alisema baadhi ya vyama vya siasa vinailalamikia kamati yake kutoa taarifa ya kumtaka Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Serikali (CAG), Ludovick Utouh kuvikagua vyama hivyo.
Alisema iwapo kuna vyama visivyopendezwa na suala hilo, vinatakiwa kuacha kupokea fedha za umma ili visikaguliwe.
Makamu huyo alisema tangu PAC iagize suala hilo, imejenga chuki kwa baadhi ya viongozi wa vyama huku akisisitiza kwamba hadi Januari mwakani kamati itaviita vyama vyote na kuvihoji ili kujua fedha za umma zilivyotumika.
Filikunjombe alisema hadi sasa ni vyama vinne vilivyokabidhi ripoti zao katika ofisi ya CAG ambavyo ni CUF, TLP, CCM na NCCR-Mageuzi.

Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa