Mkuu wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi akifungua mafunzo.
Mhandisi Magessa akielezea mfumo huo wa jua kwa washiriki.
Moja ya vifaa walivyotengeneza wakufunzi walipokuwa wakijifunza.
Ally Jakaya akifanyiwa interview.
Na Andrew Chale, Bagamoyo
Mkuu
wa Wilaya ya Bagamoyo, Ahmed Kipozi amewataka wananchi wa wilaya hiyo
hasa vijijini kuchangamkia fursa ya kuweka umeme nuru utokanao na
jua maarufu kama Solar, ilikuboresha maisha yao na maendeleo kwa ujumla.
Kipozi
amesema hayo mjini Bagamoyo wakati wa hafla ya kufungua mafunzo maalumu
ya umeme huo kwa mafundi umeme, wadau na wauzaji wa vifaa vya umeme na
vijana mbalimbali ndani ya wilaya hiyo ambapo mafunzo hayo
yaliyoratibiwa na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).
Akielezea
kufarijika na mafunzo hayo ndani ya Wilaya yake, Kipozi amesema “Ni
fursa ya kipekee kwa washiriki kutumia ujuzi huu kwani utaboresha
maisha yenu na pia kwa vijiji vitanufaika na umeme huu wa nuru”
amesema.
Na
kuongeza kuwa, kwa fursa hiyo anaamini matumizi ya kukata miti hovyo
yatapungua na baadala yake wananchi watanufaika na huduma hiyo endapo
wataichangamkia.
“Nawaomba
wananchi hasa mulio vijijini kuchangamkia fursa hii ya umeme nuru, pia
nawapongezeni wakufunzi na wandaaji kwa kuja muda muafaka kwani
mafunzo haya ni mipango endelevu ambayo itasaidia kusambaza teknolojia
ya nishati mbadala vijijini sambamba na kuwahamasisha wananchi kutumia
nishati zitokanazo na teknolojia ya nishati jadilifu” alimalizia
Kipozi.
Kwa
upande wake, mkuu wa mafunzo hayo ya umeme nuru, Mhandisi, Finiasi
Magessa alisema mafunzo hayo yatasaidia kuboresha maisha ya watanzania
mbalimbali hasa wa vijijini ilikufikia malengo ya MKUKUTA, ili kila
Mwananchi apate umeme wa uhakika na gharma nafuu ifikapo 2015.
Aidha,
wanamafunzo wanatarajia kufaanya kwa vitendo kwa kufunga umeme nuru
katika shule na nyumba za walimu za Sekondari Kiwangwa, Matipwili na
Kibindu, huku mafunzo hayo yakitaraajia kumalizika Novemba Sab, mwaka
huu.
0 comments:
Post a Comment