Home » » MILIONI 10 YATOLEWA KUSAIDIA SHULE YA WAVULANA BAGAMAOYO

MILIONI 10 YATOLEWA KUSAIDIA SHULE YA WAVULANA BAGAMAOYO

SHIRIKA la nyumba nchini limeipiga jeki ya sh. Milioni 10 shule ya sekondari ya wavulana ya Marian wilayani Bagamoyo kwa ajili ya ukamilishaji ujenzi wa jengo moja la ghorofa tano ambapo itakapokamilika mwishoni mwa mwaka huu itatoa fursa ya vijana wengi wa kidato cha kwanza na tano wanaokosa nafasi kupata madarasa ya kusomea mwakani.

Mbali na kutoa fedha hizo, pia shirika hilo kupitia kwa Mkurugenzi wake mkuu Nehemia Msechu jana limewahamasisha wazazi na walezi kuchangia ujenzi huo ambapo katika harambee ya papo kwa papo zilipatikana sh.Milioni nane na mifuko ya saruji 300.

 Akizungumza na wazazi na walezi wa watoto wanaosoma kwenye shule hiyo huko wilayani Bagamoyo, Msechu amesema ni vema jamii ikajenga tabia ya kuchangia katika shughuli za maendeleo na siyo kwenye harusi,ngoma na kipaimara pekee

Msechu amesema uridhi wa vijana katika wakati huu wa utandawazi ni elimu na si mali wala fedha hata kama mzazi wake ni tajiri kiasi gani asipokuwa na utaalamu wa kielimu hakuna chochote atakachokiweza kukimudu kuboresha maisha yake katika suala Zima la maendeleo.-

Mkurugenzi huyo wa shirika la nyumba la Taifa pia amewaasa wanafunzi wanaohitimu kidato cha nne kuwa makini na kufuata maadili mema wanayofundishwa shulen,na watambue ipo changamoto ya dawa za kulevya nchini tatizo ambalo wanapaswa wajiandae kiakili na kimwili kwenda kukabiliana nalo huko mitaani watakapokuwa baada ya kihitimu elimu yao.

Awali wanafunzi 110 wanaohitimu kidato cha nne katika sekondari hiyo walimueleza Msechu kuwa kutokana na elimu bora inayotolewa shuleni hapo kumekuwepo na changamoto ya wazazi wengi kupeleka watoto wao hapo lakini kutokana na uhaba wa madarasa imekuwa vigumu kuchukuliwa wengi hali ambayo imekuwa ikileta malalamiko ya kunyimwa nafasi kumbe miundombinu ni chache

katika risala yao iliyosomwa na Yusuf Omar wahitimu hao wamesema wao kama mabalozi wa elimu ili kukabiliana na changamoto hiyo wamechangia mifuko 150 ya saruji ili kuharakisha ujenzi wa madarasa unaoendelea na kuweza kuongeza idadi ya vijana hapo mwakani,pia walitoa changamoto kwa wadau wa elimu nchin kuongeza maabara zenye uwezo wa vitabu na vifaa vya kisasa ili kuzalisha wahitimu wanasayansi halisi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa