Home » » MAREFA WAPIGWA MSASA

MAREFA WAPIGWA MSASA

Waamuzi wa mchezo wa soka Mkoa wa Pwani wametakiwa kuifanya kazi hiyo kwa kufuata misingi ya haki ili kuwezesha timu zetu kufanya vizuri katika mashindano mbalimbali yanayohusiana na mchezo wa soka nchini.

Akizungumza katika ufungaji wa mafunzo ya marefa  Katibu wa Chama cha Marefa Tanzania, BW.CHARLES NDAGALA amewapongeza marefa hao kutoka maeneo mbalimbali ya mkoa wa Pwani kwa kujitolea kifedha na kuweza kuhudhuria mafunzo hayo.

BW.NDAGALA amebainisha kuwa anawashukuru Chama Cha Soka katika Mkoa wa Pwani, Kwa kuweza kuchangia gharama mbalimbali kuwezesha kufanyika kwa semina hiyo kwa lengo la kuwapiga msasa waamuzi hao ili waweze kufanya kazi yao kwa weledi.

Naye mgeni rasmi katika ufungaji wa mashindano hayo, Mwenyekiti wa kamati ya mashindano ya COREFA, GODFREY NYANGE KABURU amewataka waamuzi hao kuzingatia misingi ya haki wanapotekeleza majukumu yao, na hasa kutokana na klabu kutumia fedhaa nyingi kuandaa mashindano.

NYANGE amewaeleza waamuzi hao kuwa mashindano hayo yatawasaidia  kufanya maamuzi sahihi wanapokuwa wanachezesha mashindano mbalimbali na hivyo kusaidia kukuza kiwango cha mchezo huo nchini.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa