Home » » Kiwanda cha kuua mbu cha mkuna JK

Kiwanda cha kuua mbu cha mkuna JK

RAIS Jakaya Kikwete amesema kuwa atafurahi iwapo kiwanda cha kuzalisha dawa za kuulia viluwiluwi vya mbu wanaoeneza malaria kitaanza rasmi ifikapo Desemba 9, mwaka huu.
Kikwete alisema hayo jana alipokuwa akiweka jiwe la msingi katika kiwanda hicho kilichopo Kibaha, Pwani ambapo alisema ugonjwa wa malaria ni tishio nchini na duniani kote.
Alisema serikali imekuwa ikifanya jitihada kupunguza vifo vya kina mama wajawazito na watoto chini ya miaka mitano.
Kikwete alisema kiwanda hicho kilianza kutoa dawa katika kata 72 za Jiji la Dar es Salaam, hivyo kitasaidia kunusuru maisha ya watu.
Alisema, wazo la ujenzi wa kiwanda hicho alilipata mwaka 2009 alipokwenda Cuba, baada ya kuiona teknolojia hiyo ya kuua vijidudu vya malaria na kuifurahia.
Awali, Mwenyekiti wa Bodi ya Shirika la Taifa la Maendeleo (NDC), Dk. Chrisant Mzindakaya, alisema ujenzi wa kiwanda hicho hadi kukamilika utagharimu dola za Marekani mil. 22.3 na sh bil. 5 zilizotolewa na serikali.
Alisema kiwanda hicho kiko nyuma ya mpango wa utekelezaji wa mradi kwa miezi 14, kazi inayoendelea sasa ni ufungaji wa mitambo na maandalizi ya kupeleka wataalamu wa Kitanzania kwenye mafunzo kwa ajili ya uzalishaji.
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa