MKAZI wa Tengerea, wilayani Mkuranga, Pwani, Hassan
Mohammed (42) maarufu kwa jina la Nailoni, anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za
kumuua binti yake kwa kumkata kwa panga.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Pwani, Ulrich Matei
alisema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Septemba 20 mwaka huu
katika Kijiji cha Tengerea, ambako Mohammed alimuua bintiye, Amina Hassan (17)
kwa kumkata panga shingoni na kichwani.
Kamanda Matei alieleza uchunguzi wa awali umebaini
mtuhumiwa huyo ana maradhi ya akili. Mwili wa marehemu umehifadhiwa Hospitali
ya Wilaya ya Mkuranga kwa uchunguzi.
Katika tukio lingine, Hamisi Maliki, mkazi wa
Hoyoyo ameuawa na wananchi baada ya kutuhumiwa kuvunja duka la Edward Mikael,
katika Kijiji cha Mivule Wilaya ya Mkuranga.
Katika tukio la tatu, mtu mmoja amefariki dunia na
mwingine kujeruhiwa baada ya gari T 748 ADX Scania kupasuka tairi la nyuma
kulia na kupinduka katika Kijiji cha Msolwa Wilaya ya Bagamoyo.
Kamanda Matei alimtaja aliyefariki dunia kuwa ni
Marid Mtamwa, mkazi wa Njombe na majeruhi ni Erick Mvula, utingo wa gari hilo
ambaye amelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya Tumbi.
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment