Home » » Kuishi Kibaha sasa ni kwa mkataba!

Kuishi Kibaha sasa ni kwa mkataba!

WILAYA ya Kibaha imeanzisha utaratibu wa kutumia mikataba ya kusajili watu wageni wanaohamia kimakazi katika vijiji na mitaa mbalimbali kwa lengo la kupunguza na kuondoa kabisa migogoro ya ardhi wilayani humo.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake,mkuu wa wilaya ya Kibaha Halima Kihemba amesema kumekuwepo na kutokuelewana mara kadhaa kwa baadhi ya wakulima na wafugaji katika maeneo mengi ya vijijini na uchunguzi ukabaini migogoro hiyo inatokana pia na watu kuhamia na kujichukulia maeneo bila kufuata taratibu ya matumizi ya maeneo husika.

Amesema uingiaji huo wa kiholela unamfanya mtu kujiamulia afanye nini katika eneo analolimiliki hata kama matumizi ya ardhi hiyo siyo anayotaka kutumia na hivyo kuleta kutokuelewa kwa upande wa pili mfano anayehamia ni mkulima anaanza kulima wakati wenyeji wake ni wafugaji.

Kutokana na uingiaji huo wa kujiamualia Kihemba amesema sasa wilaya hiyo kupitia halmashauri zake mbili mjini na vijijini wamebuni utaratibu wa kutumia mikataba ambapo mgeni yeyote akifika atapaswa kujisajili na kuishi kikanuni kama mkataba huo unavyomuelekeza na endapo atakiuka atawajibishwa moja kwa moja.

Kihemba alitaja moja ya sharti lililopo kwenye mkataba huo unawataka wageni wote kujisajili kuwa ni kuheshimu miundombinu yote iliyopo kijijini ama kwenye mtaa na pia atambue ardhi ni mali ya kijiji au mtaa husika.

Naye Mkurugenzi wa hamashauri ya Kibaha vijijini Fatuma Selemani amesema hivi karibuni kumekuwepo na migogoro ya mara kwa mara katika kata za Ruvu,Kwala,Dutumi na hivyo kupitia mpango huo wa kusaji wageni kimkataba utaweza kupunguza kabisa hali hiyo.

Fatuma aomengeza kuwa mipango ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji vinne vya Magindu,Gumba,Lukenge na Mpiji vimeandaliwa kwa mwaka 2010 na kwamba vijiji vingine vitatu vya Kwala,Mperamumbi na Msua viko kwenye maandalizi ya mwisho mwaka 2012,2013 kuandaa mpango wa matumizi ya ardhi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa