Home » » MWANAMITINDO WA KIMATAIFA FLAVIANA MATATA AZINDUA JENGO LA MADARASA MAWILI ALIYOYAJENGA YA SHULE YA MSINGI MKOANI PWANI

MWANAMITINDO WA KIMATAIFA FLAVIANA MATATA AZINDUA JENGO LA MADARASA MAWILI ALIYOYAJENGA YA SHULE YA MSINGI MKOANI PWANI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Mwanamitindo wa Kimataifa afanyae kazi zake nchini Marekani, Flaviana Matata (wa tatu kulia) akikata utepe kuashiria uzinduzi wa jengo alilojenga la madarasa mawili na ofisi ya mwalimu mkuu wa shule ya msingi kwa shule ya msingi Msinune, iliyopo kata ya Kiwangwa wilayani Bagamoyo Mkoa wa Pwani jana.
Mwanamitindo wa Kimataifa afanyae kazi zake nchini Marekani, Flaviana Matata kushoto akikabidhi mipira kwa wanaafunzi wa shule hiyo, Flaviana ni mlezi wa shule hiyo.
Mwanamitindo Flaviana akionesha cheti cha heshima alichotunukiwa na uongozi wa kata ya Chiwangwa baada ya kuwajengea majengo ya shule.
Flaviana akipokea zawadi ya mbuzi kutokea kwa Mwenyekiti wa Kijiji cha Msinune, Ramadhan Mtokeni (kushoto) huku Diwana wa kata ya Chiwangwa (kulia) Malota Kwagga na Afisa elimu wa kata hiyo Blasius Alphonce kulia kwa diwani na Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Msinune, Alex Lugaigalila wakiangalia.
Flaviana akiwahoji wanafunzi hao maendeleo yao ya masomo shuleni hapo.
Flaviana akiwa amekalia moja kati madawati 45 ambayo aliyatoa kwa shule hiyo mwaka jana, kulia ni Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Msinune, Alex Lugaigalila na kushoto ni Afisa elimu wa kata hiyo Blasius Alphonce.
Flaviana akipokea cheti cha heshima kutokea kwa Mtendaji wa Kijiji cha Msinune, Memory Mbangwa cha kutambua mchango wake huo.
Flaviana akiwa na watendaji wa kijiji hicho na kata pamoja na wanakijiji waliojitokeza siku hiyo.


Alipata wasaha wa kupiga picha na wanafunzi pia siku hiyo ambao walimpongeza kwa msaada wake huo



Na Evance Ng’ingo

MWANAMITINDO wa kimataifa afanyaye shughuli zake nchini Marekani, Flaviana Matata madarasa mawili ya shule za msingi iliyopo katika kijiji cha Msinune kilichopo kata ya Kiwangwa Wilaya ya Bagamoyo mkoani Pwani.

Flaviana alipewa jukumu la ulezi wa shule hiyo na wanakijiji wa Msinune mwaka 2014 wakati alipoenda kuwasaidia wanafunzi mabegi ya shule, walimpatia jukumu la kuwatengenezea vyoo, ofisi na nyumba za walimu pamoja na kumalizia ujenzi wa darasa.

Tangia alipopewa majukumu hayo alianza kwa ujenzi wa vyoo vya walimu na wanafunzi, na juzi alienda kukabidhi jengo la madarasa, darasa la saba na la sita pamoja na ofisi ya Mkuu wa Shule.Akizungumza wakati wa makabidhiano hayo Flaviana alisema, tangia alipopewa jukumu la ulezi wa shule hiyo amekuwa akihangaika huku na kule kupata fedha za kutatua kero za shule hiyo.

Alisema, kwa kufanikiwa kukabidhi jengo hio la madarasa anaona kuwa ameshiriki kikamilifu katika kutekeleza jukumu lake kama mwanajamii la kusaidia maendeleo ya elimu kwa jamii iliyokuwa na uhitaji mkubwa.

Alisema” sisi kama vijana kama watanzania tunalo jukumu la kujitokeza na kusaidia maendeleo ya elimu na sekta nyingine muhimu nchini kwa kuwa hili sio jukumu la serikali peke yake, sasa nimeshatengeneza vyoo vya walimu na wanafunzi na leo nakabidhi darasa”

Kwa upande wake Mwalimu Mkuu wa shule hiyo, Alex Lugaigalila alisema ujenzi wa darasa huo utawaongezea ufanisi wanafunzi katika masomo yao huku akibainisha wazi ushiriki wa Flaviana kwenye maendeleo ya shule hiyo umeongeza hamasa ya wanafunzi kusoma.

Kwa upande wake Afisa wa elimu wa Kata hiyo,Blasius Alphonce alisema kwa ujenzi wa jengo hilo, Flaviana amesaidia jitihada za serikali katika kuendeleza elimu kwenye kata hiyo yenye vijiji vitano.

Jengo hilo la darasa lililojengwa lina vyumba viwili vikubwa vilivyoezekwa kwa bati huku likuwa na madirisha makubwa yanayowezesha kupitisha hewa na chumba cha mwalimu mkuu.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa