Home » » TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: RAIS ATENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI KIBAHA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI: RAIS ATENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI KIBAHA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 



JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

 OFISI YA RAIS

Anuani ya Simu: “TAMISEMI”
Simu Na: (026) 2322848, 2321607
 2322853, 2322420
Nukushi: (026) 23221
16, 2322146
2321013 
Barua pepe: ps@poralg.go.tz

Tawala za Mikoa na
Serikali za Mitaa,
S.L.P. 1923,
DODOMA.


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Rais wa Jamhuri  ya Muungano wa Tanzania, Mhe. John  Pombe Magufuli ametengua  rasmi  nafasi ya   Mtendaji  Mkuu wa Shirika  Elimu Kibaha  Dkt. Crispin  Mpemba  ili kupisha uchunguzi wa tuhuma mbalimbali za kiutendaji zinazomkabili.
Akijibu swali la Waandishi wa Habari waliotaka kupata ufafanuzi juu ya hatma ya tuhuma mbalimbali zinazolikabili Shirika la Elimu Kibaha ambazo zimekuwa zikiandikwa kwenye vyombo vya habari kwa muda mrefu sasa, Mhe. Simbachawene alisema kutokana na kuwepo kwa tuhuma mbalimbali za uendeshaji, Mhe. Rais  Magufuli tarehe  4/3/2017  ametengua rasmi nafasi ya Mtendaji huyo ili kupisha uchunguzi.
“ Ni kweli tuhuma juu ya uendeshaji wa Shirika la Elimu Kibaha likiwemo suala la Mikataba iliyoingiwa na Shirika hilo zimekuwepo kwa muda mrefu sasa. Sisi kama Wizara hatukutaka kukurupuka kufanya maamuzi na tukaamua kuunda kikosi kazi ili kufanya uchunguzi na matokeo ya uchunguzi huo  yanapelekea kuwepo kwa hoja  zinazohitaji uchunguzi zaidi.  Hivyo, ili uchunguzi huo uweze kufanyika  Mhe. Rais amemsimamisha kazi Mtendaji huyu Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha ili kupisha uchunguzi wa kina dhidi yake. Alisema Mhe. Simbachawene
Alisema uamuzi wa kumsimamisha umechukuliwa kwakuwa tuhuma za awali zilizojitokeza dhidi yake zinajenga hoja ya kuhitajika kufanyika kwa uchunguzi zaidi.
Kwasasa nafasi ya Mtendaji Mkuu wa Shirika la Elimu Kibaha inakaimiwa hadi hapo  uchunguzi utakapokamilika.

Rebecca Kwandu
Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini,
Ofisi ya Rais,
Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa.
06/03/2017.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa