Home » » WAKUU WA IDARA WASIKIMBIE WANANCHI

WAKUU WA IDARA WASIKIMBIE WANANCHI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

WAKUU wa Idara katika Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, wametakiwa kuachana na utaratibu wa kutuma wawakilishi kwenye mikutano ya wananchi kwani kufanya hivyo ni kuibua hofu ya maendeleo kwa wananchi.
Baadhi ya wakuu wa idara, wamekuwa wakituma wawakilishi mara kwa mara katika mikutano na hivyo wananchi kukosa majibu ya moja kwa moja kutoka kwa viongozi wao wa serikali.
Wito huo umetolewa hivi karibuni na Mbunge wa Kisarawe, Selemani Jafo, wakati akizungumza na wakazi wa kitongoji cha Masimba, ambako alisema kuwa uwakilishi huo umekuwa ukimkera kwani unasababisha wananchi kukosa imani na viongozi waliopo madarakani.
Alisema kitendo cha baadhi ya wakuu wa idara kutuma wawakilishi, kimekuwa kikisababisha hofu ya maendeleo kwa wananchi hasa kwenye utekelezaji wa miradi mbalimbali, kwa kukosa takwimu na kushindwa kujibu namna ya utatuzi wa changamoto.
“Nakushukuru Ofsa Elimu wa Wilaya kwa maana kila ninapokupa taarifa ya kushiriki na mimi kwenye mikutano amekuwa akifanya hivyo na kusaidia kutoa majibu ya moja kwa moja kwa maswali ya wananchi, uwakilishi kwa baadhi ya watendaji umekuwa kikwazo cha maendeleo ambacho naendelea kupiga vita tabia hii inayoleta hofu kwa wananchi,” alisema Jafo.


Hivi karibuni ujenzi wa nyumba ya mwalimu katika kitongoji cha Masimba ulikwama kwa zaidi ya miezi sita kutokana na wakandarasi kuhitaji fedha kubwa tofauti na iliyotengwa na Halmashauri.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa