Home » » RC MAHIZA AHIMIZA CHANJO YA SURUA NA RUBELLA

RC MAHIZA AHIMIZA CHANJO YA SURUA NA RUBELLA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

MKUU wa Mkoa wa Pwani, Mwantum Mahiza, amewataka wananchi kushiriki kikamilifu kwenye zoezi la chanjo ya surua na rubella inayoanza leo hadi Oktoba 24 mwaka huu na kwamba hazina madhara.
Mahiza, alitoa wito huo wakati akizungumza na waandishi wa habari pamoja na viongozi wa Mkoa kuhusiana na zoezi hilo, alisema viongozi wa ngazi zote mkoani hapa, wanatakiwa kushiriki kikamilifu kuhamasisha wananchi kujitokeza kwenye vituo vilivyopangwa.
“Viongozi wa serikali za mitaa na viongozi wa ngazi zote pamoja na wa madhehebu yote, tuwahamasishe wananchi wajitokeze, dawa hizi hazina madhara yoyote na chanjo hizi ni kinga kwa magonjwa mengine,” alisema Mahiza.
Aidha, alisema zoezi hilo litaambatana na utoaji wa dawa za matende na mabusha, chanjo ya surua rubella, matone ya vitamin A na dawa za minyoo.
Awali akitoa taarifa kuhusiana na zoezi hilo, Mratibu wa chanjo ya watoto mkoani Pwani, Abbas Hincha, alisema chanjo ya surua na rubella walengwa ni 458,000 vitamin A 390,000 matende na mabusha 850,000.
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa