Home » » SEKONDARI YA LUGOBA YAJITAJI MIL. 9/-

SEKONDARI YA LUGOBA YAJITAJI MIL. 9/-

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

SHULE ya Sekondari Lugoba wilayani hapa Mkoa wa Pwani, inahitaji sh milioni tisa kwa ajili ya ununuzi wa mashine ijulikanayo kama ‘Embozer’ kwa ajili ya kuchapishia mitihani ya wanafunzi wasioona.
Hayo yamebainishwa na Mkuu wa shule hiyo, Abdallah Sakasa, wakati wa mahafali ya 23 ya kidato cha nne, ambako alibainisha endapo mashine hiyo itapatikana, itapunguza gharama zinazotumika kwa sasa.
Sakasa, alisema mashine hiyo ambayo inapatikana Nairobi Kenya,  itatumika kama ‘printer’ ikiunganishwa kwenye kompyuta na kutoa herufi nundu zinazotumiwa na wanafunzi hao.
“Changamoto hii ya upatikanaji wa mashine ya kuchapia hurufi nundu bado ni kubwa katika shule yetu, kwani mashine moja inauzwa sh milioni 1.8 na sisi tuna upungufu wa mashine tano,” alisema.
Aidha, aliainisha changamoto nyingine kuwa ni pamoja na gharama za kemikali na vifaa vya maabara, kutokana na kuwepo kwa wanafunzi wengi wanaosoma masomo ya sayansi katika shule hiyo.
Shule hiyo ambayo ilianzishwa mwaka 1989, sasa ina wanafunzi 1,367 wasichana wakiwa 674 kidato cha kwanza hadi cha sita, ambako wahitimu wa kidato cha nne mwaka huu wakiwa 151.
Chanzo;Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited
Copyright © 2012. Pwani Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za Mikoa